JE! UNAJISIKIA KUWA HAUFAI NA KUWA NA MISUKOSUKO?

David Wilkerson (1931-2011)

Ikiwa umewahi kuwa na nyakati za kujisikia kama haufai na kuwa na misukosuko, basi Zaburi 77 iliandikwa kwako. Mwandishi wa Zaburi hiyo, mtu mmoja aitwaye Asafu, alikuwa Mlewi kutoka kwenye ukoo wa makuhani huko Israeli. Alikuwa pia mwimbaji na aliwahi kuwa mkurugenzi aliyechaguliwa na Daudi. Kwa ujumla, Asafu aliandika Zaburi kumi na moja na zilikuwa zimejaa mafundisho ya haki kwa watu wa Mungu.

Asafu aliandika Zaburi ya 77 baada ya kuanguka katika shimo la kutisha na la kukata tamaa, na hali yake ikakua mbaya sana kwamba hakuwa na faraja: "Roho yangu ilikataa kufarijiwa" (77:2). Hata hivyo Asafu alikuwa mtu anayeomba. Tunaona hili katika Zaburi hiyo kama alivyosema: "Nilimlilia Mungu kwa sauti yangu ... naye alinitega sikio" (77:1). Nina hakika Asafu amesikia ushuhuda wa Daudi sawa sana katika Zaburi ya 34: "Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako wazi kuelekea kilio chao" (34:15).

Asafu alijua hadithi ya Daudi ya jinsi alivyohitaji kimbia kutoka Gati ikimbia ghadhabu ya Sauli. Alijisikia kama ameshindwa na  akamulilia Mungu kwa uchungu na alikuwa amemtolewa kabisa. Kwa kweli, Mungu aliweka wimbo katika moyo wa Daudi. Katika Zaburi ya 40 Daudi aliandika wimbo mpya wa imani ambayo kwa hakika uliiweka katika mikono ya Asafu kama ushuhuda: "Alikisikia kilio changu. Alinitowa kutoka shimo la kutisha ... na akayisimamisha miguu yangu juu ya mwamba" (40:1-2).

Je!Hadithi ya Asafu inaelezea vita vyako vya kiroho? Mtu wa Mungu huyo mwaminifu, mwenye kuomba, alikuwa akikabiliwa na unyogovu na kunaonekana kwamba hakuna njia nyingine ya kupitoka. Lakini alihitimisha, "Njia za Mungu hazijulikani. Sijui ni kwa nini aliniruhusu nipate kukata tamaa kama hiyo, lakini ninaweza tu kufurahi kwamba amenifanya huru."

Daudi akasema, "Nimemtafuta Bwana, naye akanisikia, akaniokoa kutokana na hofu zangu zote" (Zaburi 34:4). Kwa kweli, Roho Mtakatifu atakufariji katika nyakati zako za giza na kukusaidia kurudisha furaha yako, amani na kupumzika wakati unapomtafuta.