JE! UKO KWENYE MWISHO WAKO MWENYEWE?

David Wilkerson (1931-2011)

Roho ya kukata tamaa ni silaha ya Shetani yenye nguvu sana dhidi ya wateule wa Mungu. Mara nyingi, hutumia ili kutushawishi kama tumeleta ghadhabu ya Mungu juu yetu wenyewe, kwa kutoweza kupima viwango vyake vitakatifu. Lakini mtume Paulo anatuhimiza tusianguke ndani ya mtego wa shetani: "Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikira zake" (2 Wakorintho 2:11).

Paulo anasema, "Unapaswa kuona kukata tamaa kwako kwa uhakika - silaha ya pepo - mshale ambao Shetani anakurushia wewe ili uwe na wasiwasi mwenyewe. Anajua hawezi kukujaribu kugeuka nyuma mbali ya Yesu, kwa hiyo anakudanganya kupitia uongo mbaya ili akufanye ufikiri kamwe hutakuwa mzuri wa kumtumikia Kristo."

Roho ya Mfalme Daudi ililetwa chini kwa ukamilifu, kuvunjika, kuomboleza, hisia ya shida. Alihisi kuwa kavu na kuwa tupu, bila ya uongozi: "Moyo wangu unapwita-pwita, nguvu zangu zimeniacha; nuru ya macho yangu nayo imeniondoka." (Zaburi 38:10). Daudi anasema, "Maono yangu na ufunuo wa Bwana vimeniacha na siwezi kumfikia Mungu kama nilivyofanya mara moja."

Mimi mwenyewe ninajua jinsi Daudi alivyohisi. Nimepata baraka nyingi kwa njia ya huduma yangu lakini mara nyingi, ndani ya siku za matukio makubwa, nimesumbuliwa na kukata tamaa. Sisi ni malengo ya nguvu za kuzimu wakati wa ushindi mkubwa wa kiroho.

Kuna idadi kubwa ya wanaume na wanawake waliojitolea ambao Bwana alitumia kwa nguvu, na kila mmoja wao alijitahidi kupitia kukata tamaa kali. Kwa mfano, mhubiri mkuu wa Uingereza C. H. Spurgeon aliwaongoza watu wengi kwa Kristo kupitia mahubiri yake yenye nguvu lakini alipata mateso mabaya ya kuchukiza.

Kitu cha kwanza Roho Mtakatifu anafanya katika nyakati hizo ni kukukumbusha yote ahadi ya thamani ya Yesu. Atakuzidisha nafsi yako na ahadi hizo na roho yako itaongezeka ndani yako. Kazi ya Roho Mtakatifu ni kufuta uongo wa adui na kuleta moyo kutoka juu! Uhakikishwe kwamba wote wanaomngojea Bwana watapata ahadi zake za utukufu!