IKIWA SIWASAIDIA, NI NANI ATAYEWASAIDIA?

Nicky Cruz

Kama wafanyakazi wenzangu na mimi tukiwahudumia wale waliokuja kwa ajili ya maombi mwisho wa huduma, niliona bibi mwenye umri mkubwa akiwa na watoto wawili wadogo katika mikono yake. Alikuwa akalia na kutuomba tuombee wajukuu wake.

"Omba ili Mungu atawalinda," alilia akiwaweka chini. "Tafadhali omba ili waweze kukua salama na furaha, wasiingie kwenye vikundi vya waharifu na madawa ya kulevya. Tafadhali?"

Moyo wangu ulivunjika mwanamke huyu na wajukuu wake, hivyo wasio na hatia na kuwa wazuri. Macho yake alililia msaada, kwa uongozo, kwa aina yoyote ya msamaha kutoka kwa maumivu na upungufu wa maisha katika ghetto. Nikamkumbatia na kisha nikinama chini kwa ajili ya watoto. Aliendelea kuinuka na kulia wakati wote.

Kuna watu wengi ulimwenguni hapa ambao wamepoteza na hujitenga  na kuumizwa, watu ambao hawana mahali pa kugeukia na hawajui jinsi ya kuepuka ushindi wa Shetani. Yesu ndiye pekee ambaye anaweza kuwasaidia. Wote wanahitaji mtu wa kuwaelekeza kuelekea Msalabani, mtu w kuwachukua kwa mkono  kuajali kikamilifu na kuwaongoza katika mikono ya Muumba wao, mtu wakushika na kuwapenda katika ufalme.

Nilipomaliza kuomba, niliweka mkono wangu juu ya mwanamke mzee na kumbusu kwenye paji la uso. "Usijali," nikamwambia. "Kila kitu kitakuwa sawa. Yesu anaelewa."

Kuna kitu juu ya kuangalia kwa kutokuwa na tumaini, kukata tamaa, na huzuni kamili ambayo huleta ujumbe wa injili nyumbani kwako kwa njia ambayo hakuna kitu kingine chochote kinaweza. Maisha yako anachukua hisia mpya ya kusudi na uharaka na unataka kutumia wakati wote wa maisha yako kuonesha imani yako na kuweka mioyo ilio tekwa kuwa huru.

Kufikia watu kwa ajili ya Yesu ni maisha yangu. "Bwana akamwambia mtumwa, 'Toka nje uende barabarani na mipakani, ukawashurutishe kuingia ndani, nyumba yangu ipate kujaa'" (Luka 14:23). Ninakuhimiza kujiunga na mimi na kujiuliza swali hili: Ikiwa siwasaidia, ni nani atakayewasaidiya?

Nicky Cruz, mwinjilisti wa kimataifa aliyejulikana na mwandishi mkubwa, alimgeukia Yesu Kristo kutoka kwenye maisha ya vurugu na uhalifu baada ya kukutana na David Wilkerson huko New York City mwaka 1958. Hadithi yenye kushangaza ya kuokoka kwake ilisemwa mara ya kwanza katika Musaraba na Kisu kinachomoka ( Cross and Switchblade) na David Wilkerson na kisha baadaye katika kitabu chake chenye kuuzwa vizuri zaidi, kiitwaco:Kimbiya , Mtoto, Kimbiya (Run, Baby, Run).