HUFANYA UDHAIFU KUWA UJASIRI KAMA SIMBA

Jim Cymbala

Mfalme Daudi alitaka kujenga hekalu huko Yerusalemu na kujenga jengo la ajabu kwa ajili ya Mungu, lakini Bwana akamwambia kuwa hawezi kuwa yeye atakalofanya hilo. Badala yake, Bwana akachagua mtoto wake Sulemani. Maafisa wote wa Israeli walikusanyika Yerusalemu na Daudi alitangaza mpango wa Mungu. "[Mungu] akaniambia: 'Sulemani mwana wako ndiye atakayeijenga nyumba yangu na nyua zangu'" (1 Mambo ya Nyakati 28:6).

Uchaguzi wa Mungu ulikuwa wazi. Je! Ikuwa rahisi, na wenye kuwa sawa? Daudi alikuwa tayari amepokea mipango ya ujenzi kutoka kwa Mungu mwenyewe na kukusanya vifaa kama vyote vya ujenzi. Sulemani yote alipaswa kufanya ilikuwa ni kuanza tu. Lakini mara nyingi kuna mahali pa kushindwa. Daudi alielewa shida inayokabiliwa mwanawe. Sulemani: "Uwe hodari kwa kutenda hivyo" (mstari wa 10). Na "kuwa na nguvu na ujasiri, na kufanya kazi. Usiogope au ukate tamaa, kwa kuwa Bwana Mungu, Mungu wangu, yu pamoja nawe. Hatakukupungukia au kukuacha kufikia kazi itakapomalizika" (mstari wa 20).

Licha ya ukweli kwamba Sulemani alikuwa chaguo la Mungu na kwamba alikuwa na maagizo kamili na vifaa vyote muhimu, bado aliendelea kuwa na woga wazamani uliotufanya kuwa viwete kwa kutokufanya kazi. Ujumbe, tafsiri ya kisasa ya Bibilia, hutafusiri msitali wa 10, "Na ufanye hivyo!" Hakuna mtu anasema kwamba hapatakuwa pengamizi au shida, lakini ni kwa njia ya Roho kwa imani na ujasiri ambao tunaweza kuwa na ujasiri na kuendelea na kazi ambayo Mungu ametuita kufanya.

Mungu ametuita sisi sote kuwa kitu fulani. Yesu alisema kuhusu wakati atakaporudi: "Jitahadharini! Kuwa macho! Kwa kuwa hamujui wakati huo utakapofika" (Marko 13:33). Lakini kwa sababu ya hofu, hatukuenda nje na kulifanya hilo.

Roho Mtakatifu ni mkuu zaidi kuliko nguvu zetu au aibu na ni mkubwa zaidi kuliko hofu yetu au kukataa au kushindwa. Nguvu zake hufanya mtu dhaifu sana kuwa shujaa kama simba (angalia Methali 28:1).

Jim Cymbala alianza Hema la Brooklyn (Brooklyn Tabernacle) akiwa na wanachama wasio zidi  ishirini katika jengo la chini katika sehemu ngumu ya mji huo. Mzaliwa wa Brooklyn, yeye ni rafiki wa muda mrefu wa David na Gary Wilkerson.