FURAHIYA KRISMASI

Gary Wilkerson

Kila mwaka wakati wa likizo nyingi, Wakristo wanajikumbusha umuhimu halisi wa Krismasi: kuja kwa Yesu! Mioyo yetu imejaa shukrani kwamba Mungu Baba alimtuma Mwokozi atufungue. Tunafurahia baraka nyingi: kuona zawadi za rangi karibu na mti kwenye chumba cha kulala; kuimba nyimbo za furaha na tenzi; kumshukuru Mungu kwa wema wake. Baadhi yetu hatafurahia kutazama "Charlie Brown Krismasi," na Linus akisema maneno kutoka Luka 2 mpaka mwisho.

Tunapaswa kushukuru kwa mioyo yetu yote kwa baraka tunazofurahia wakati wa Krismasi. Tunajua kwamba vitu vyote vyema vinatoka kwa Baba. Hata hivyo ni vyema tukijikumbusha kwa nini Yesu alikuja: kwa sababu tunapigana vita - kwa vita na nguvu za giza, na roho za pepo, na shetani mwenyewe. Ibilisi anakuja katika maisha yetu kujaribu kuiba, kuua, na kuharibu - wote katika jaribio la kutupoteza kutokana na malengo mazuri ya Mungu. Kwa kuzaliwa kwa Kristo, Mungu aliweka jeshi kubwa ili kupigana na adui kwa njia mpya - kwa kweli, Siku- ya D,au Siku inayo kuja (D-Day) kutua dhidi ya nguvu zilizoingizwa za kuzimu.

Waumini wengi hawataki kukubali vita hivi katika maisha yao lakini ni ukweli wa kibiblia kwamba adui wa roho zetu daima ni kinyume cha watu wa Mungu. Kwa hiyo, kama lengo letu wakati wa likizo juu tu ya baraka - hata mambo mazuri kama kutoa na kupokea - tunakosa athari kamili ya dhabihu ya Yesu kwa niaba yetu. Na tunakosa kwa undani, Baraka zamwisho ambazo Krismasi inatufunuliya ni zetu.

Mungu Baba alihakikisha kuwa Mwana wake mpendwa aliokolewa. Ushindi wote wa miujiza uliofurahiwa kwa jina la Yesu kwa karne nyingi umewekwa huko katika hori la ng’ombe wanyenyekevu, katika mufano wa mtoto mchanga.

Tunaposherehekea Krismasi, tuwe na shukrani kwa baraka zote za Mungu, hasa ushindi tunao kwa sababu ya kuzaliwa kwa mtoto Kristo.