FARAJA KATIKA HUZUNI

David Wilkerson (1931-2011)

Siri ya kuelewa jinsi Mungu anatuokoa kutokana na mateso yanaweza kupatikana katika kuelewa jinsi alivyookoa Israeli kutoka utumwa wao.

"Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi" (1 Wakorintho 10:11).

Kila kitu kilichotokea Israeli - utumwa wao, majaribio yao, ukombozi wao kutoka Misri - ni ushuhuda, sanamu na mifano kwa sisi leo. Hakika, ukombozi wa kimwili wa Israeli unawakilisha ukombozi wa kiroho tunawoona.

Je! Umewahi kujiuliza kwa nini Israeli haikufufuka katika uasi wakati wa utumwa chini ya Farao? Baada ya yote, alikuwa amewahimiza kufanya matofali bila majani na kuwaamuru wafanyakazi wake kuwapiga. Kwa nini Waisraeli hawakushika mambo kwa mikono yao wenyewe? Kwa hakika walikuwa na nguvu zinazohitajika, hasa baada ya mapigo kumi, wakati Misri iliharibiwa, kuwa dhaifu na kwa kuomboleza. Hata Farao alikiri, "Watu wa wana wa Israeli ni wengi tena wana nguvu kuliko sisi" (Kutoka 1:9).

Sababu za Israeli kutofanya uasi ni kwa sababu hawangeweza kufanikiwa! Ilikuwa kazi ya Mungu kuwatendea. Bwana akamwambia Musa, "Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, name nimekisikiya kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao" (Kutoka 3:7-8).

Mungu anasema waziwazi, "Najua huzuni zao." Mpendwa, kama hiyo haijakufariji katika shida yako, hakuna kingine chochote kitafanya hivyo.  Bwana anasema, "Najua mambo unaopitia, na yenye unayo hisi. Lakini hii si vita yako. Msimamizi wako wa kazi, shetani, ni mkubwa sana kwa ajili yenu, hivyo nimetelemuka chini kukuokowa."

"Mimi ni YEHOVA, nami nitawatoa ninyi mtoke chini ya mizigo ya utumwa wao, nami nitawaokoa kutoka kwa utumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyoshwa, na kwa hukumu kubwa; name nitawatwaeni kuwa watu wangu, nitakuwa Mungu kwenu" (Kutoka 6:6-7).