KUACHILIA KISASI

David Wilkerson (1931-2011)

Paulo aliandikia kanisa, “Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu; kwa maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi, mimi nitalipa, asema Bwana” (Warumi 12:19). Anasema, “Acheni kudhulumiwa. Iweke chini na uendelee. Pata uzima katika Roho.”

Walakini, ikiwa tunakataa kusamehe machungu tuliyotendewa, lazima tukabiliane na matokeo haya:

  • Tutakuwa na hatia zaidi kuliko mtu ambaye alitia jeraha letu.

  • Rehema na neema za Mungu kwetu zitafungwa. Mambo yanapoanza kuharibika katika maisha yetu, hatutaelewa kwa sababu tutakuwa katika uasi.

  • Maumivu ya mtesi wetu dhidi yetu yataendelea kutunyima amani. Atakuwa mshindi, akifanikiwa kutupa jeraha la kudumu.

  • Kwa sababu Shetani anafaulu kutupeleka kwenye mawazo ya kulipiza kisasi, ataweza kutuongoza kwenye dhambi mbaya zaidi. Tutafanya makosa mabaya zaidi kuliko kutosamehe.

Mwandikaji wa Mithali ashauri hivi: “Busara ya mtu humfanya asiwe mwepesi wa hasira; na utukufu wake ni kusahau kosa” (Mithali 19:11). Kwa maneno mengine, hatupaswi kufanya chochote hadi hasira yetu itakapopungua. Hatupaswi kamwe kufanya uamuzi au kufuata hatua yoyote tukiwa bado tumekasirika.

Katika Mathayo 5:44-45, Yesu aliwaambia wafuasi wake, “Lakini mimi nawaambia, wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi, watendeeni mema wale wanaowachukia ninyi; ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; kwa maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.”

Tunamletea utukufu Baba yetu wa mbinguni wakati wowote tunapopuuza maumivu na kusamehe dhambi tulizotendewa. Kufanya hivyo hujenga tabia ndani yetu. Tunaposamehe kama vile Mungu anavyosamehe, atatuleta katika ufunuo wa kibali na baraka ambazo hatujapata kujua hapo awali.