BILA HATIA AU AIBU

Gary Wilkerson

Agano la Kale lilikuwa na kanuni ambazo zilisema, "Ikiwa utafanya hili au hilo, Mungu atakupa uzima, lakini ikiwa hutakii, utakosa baraka za Mungu" Bila shaka, watu daima walijisikia kuwa na kiwango kidogo cha Mungu kwa sababu sheria yake ilikuwa takatifu, na kwa sababu hiyo, maisha yao yalitiwa hatia na kukata tamaa. Wakati Mungu alitupa Agano Jipya, hata hivyo, hakuanzisha mfumo mpya na sheria mpya. Badala yake, alitutuma mtu kwa ajili yetu.

Agano la Kale la Mungu halikuhitaji kubadilishwa kwa njia yoyote kwa sababu Yesu mwenyewe alikuja kama agano - baraka ya neema! Kama mfano wa Agano Jipya, anatuonyesha kuwa haiwezekani kwa uwezo wetu wa kushikiliya sheria ya Mungu; Kwa kweli, tendo lake la kwanza la huduma duniani lilikuwa ni kufanya sheria ya Mungu iwe vigumu zaidi kwetu. Alifanya hivyo ili kutuonyesha jinsi hatuwezi kuiweka bila neema na nguvu zake.

Katika kile kinachojulikana kama Mahubiri ya Mlimani, Yesu alizungumza juu ya amri ya kutoua: "Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu" (Mathayo 5:22). Alifanya sawa juu ya uzinzi: "Kila mtu atazamaye mwanamke kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake" (5:28). Lakini katika mahubiri hayo alielezea jinsi inaonekana kutembea kama wafuasi wake na kuishi maisha ya baraka na ushindi.

Chini ya Agano Jipya, sheria ya Mungu haikuwa kiwango cha nje cha kujitahidi. Badala yake, sheria yake ingeandikwa mioyoni mwetu, kwa njia ya Roho Mtakatifu: "Pendo la Mungu limekwisha kumiminwa katika mioyo yetu na Roho Mtakatifu tuliyepewa sisi" (Warumi 5:5). Tunajazwa na Roho Mtakatifu - uhai wa Mungu mwenyewe - na kwa sababu ya zawadi yake kubwa, tunawezeshwa kuishi kwa yeye bila hatia au aibu.