ACHA YESU AWE KILA KITU KWAKO

David Wilkerson (1931-2011)

Bwana anatamani urafiki na watoto wake mpendwa. Anatamani kujifungia peke yake pamoja na upendo wa moyo wake. "Unapoomba, ingia katika chumbani chako, na ukisha kufunga mlango wako, omba kwa Baba yako aliye katika mahali pa siri; na Baba yako aonaye kwa siri atakuzawadiya kiwazi” (Mathayo 6:6).

Wasioamini hutamani kuona mfano halisi wa moyo wa mtumwa wa Kristo katika wale wanaojiita Wakristo. Dini nyingi leo zinavumilia dhambi na maneno kama udugu, upendo, na umoja wakati wa kuacha utakatifu wa kweli. Kinyume chake, waumini ambao hutumia wakati “katika mahali pa siri” pamoja naye huinuka na kuwasilisha ushuhuda usio thabiti kwa ulimwengu wenye njaa, wenye kungojea.

Jina la Yesu limechafuliwa ulimwenguni leo, haswa Amerika. Wanajeshi wa Kirumi walimdhihaki kwa kuweka taji ya miiba kichwani mwake, lakini taifa hili sasa linamdhihaki zaidi.

Kwa kweli, Yesu pia anakataliwa na wengi wanaodai kumtaka zaidi: Wakristo! Uliza mtu yeyote anayejiita Mkristo maswali haya: "Je! Unajihisi uhitaji wako kutoka kwa Yesu? Je! Ungetamani kumjua vizuri?” Karibu wote kati yo watatamani kujibu kwa kukubali. Lakini wengi wanapenda sifa za wanadamu na ulimbikizaji wa vitu vya juu kuliko vitu vyote. Neno la Mungu linasema, "Ikiwa mtu anapenda ulimwengu, upendo wa Baba haumo ndani yake" (1 Yohana 2:15).

Wote wanaotamani kumjua Yesu wanaweza kufanya hivyo. Neno la Mungu linasema, "Mikimtafuta Bwana Mungu wenu, na mtampata ikiwa mtamtafuta kwa moyo wenu wote na kwa roho yenu yote" (Kumbukumbu la Torati 4:29). Yesu anatamani kutumia wakati mwenyewe pamoja na wewe, kwa hivyo usijifunganiye sana katika kufanya mema ili usije kukosa kuguswa naye. Yeye ndiye uadilifu wako, nuru yako, furaha yako, amani yako, wokovu wako - kwa hivyo amruhusu awe kila kitu kwa ajili yako.