KUWAHESHIMU MAMA NA BABA ZETU
Ninapotafakari Zaburi ya 71, mara moja ninamfikiria mke wangu Chantal. Kwa miongo kadhaa, nilimwona Chantal akiwapigia simu mama na baba yake mara kadhaa kila wiki. Aliwatembelea mara kwa mara na kuwazunguka kwa uangalifu, akakaa nao hadi pumzi yao ya mwisho. Daima amekuwa kielelezo kwangu linapokuja suala la kuwajali wazazi katika changamoto zao na maumivu ya mwisho wa maisha.