Abortion

DHAHABU ILIYOFICHWA KWENYE ARDHI YETU

David Wilkerson (1931-2011)

"Kama vile uweza wake wa kimungu umetupa sisi vitu vyote vinavyohusu uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu na wema" (2 Petro 1:3).

Kwa miaka, nimedai kujazwa na Roho. Nimeshuhudia kwamba nimebatizwa kwa Roho. Nimehubiri kwamba Roho Mtakatifu ananiwezesha kushuhudia na kwamba ananitakasa. Nimeomba katika Roho, nimezungumza na Roho, nimetembea kwa Roho na kusikia sauti yake. Ninaamini kweli Roho Mtakatifu ni nguvu ya Mungu.