KUJIFUNZA KUZIBITI ULIMI

David Wilkerson (1931-2011)

Maneno tunayosema yanaonyesha yaliyo mioyoni mwetu. "Kwa maana kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake" (Mathayo 12:34). Ulimi wako unazungumza tu kilicho moyoni mwako.

Kumbuka wakati ulisema kitu kibaya wakati ulikuwa mtoto? Mama yako alikuwa haraka kwa kukurekebisha na labda akakuadhibu kwa njia fulani, sivyo? Lakini sasa kwa kuwa wewe ni mtu mzima, lazima uchukue kwa uzito maagizo ya maandiko ambayo tutatumia ulimi wetu. "Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uwovu isiotulia, umejaa sumu iletayo mauti” (Yakobo 3:8).

Kama Wakristo, lazima tukabiliane na ukweli ambao hauwezi kukamilika wa kwamba moyo ni najisi, unajisi, na mara nyingi tunazungumza mambo yasiyomcha Mungu. "Mtu mwema kutoka hazina nzuri ya moyo wake hutoa meema;, na mtu mbaya katika hazina mbaya hutoa mabaya. Lakini, mimi ninawaambia, kwamba kila neno lisilo na maana ambalo wanadamu watakalolinena, watatoa hesabu ya neon hilo siku ya hukumu. Kwa maana maneno yako utahesabiwa kuwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa” (Mathayo 12:35-37).

Hayo ni maneno ya Yesu na tunahitaji kuzingatia. Yeyote anayetaka kuishi kumpendeza Bwana lazima aende kwa uwepo wake mpaka apate maono ya utakatifu wa Mungu. Uponyaji wote, baraka zote za kweli, ushindi wote huanza katika kiti chake cha enzi, ambapo ndipo tunapoona Mungu katika utakatifu wake.

Siri ya ushindi juu ya kitu chochote katika maisha yako ni karibu na Yesu - urafiki na yeye - kumjua! Kukaribia uwepo wake kutaonyesha kile kilicho moyoni mwako. Ikiwa unakujuza au unaruhusu vitu vyene kutokuwa na maana vitokeye kinywani mwako, nenda kwa Bwana na umwombe akusaidie. Na omba Roho Mtakatifu akufanye ukubali kila wakati unapoanza kusema kitu bila kujali, bila kufikiria au kisicho na huruma.

Maombi ya moyo wako yawe, "Maneno ya kinywa change, na kutafakari kwa moyo wangu, yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, nguvu yangu na Mwokozi wangu" (Zaburi 19:14).