KWA NEEMA YA MUNGU PEKE YAKE

Gary Wilkerson

"Lakini Mungu, kwa kuwa tajiri katika rehema, kwa sababu ya upendo mwingi aliotupenda, hata wakati tulipokuwa wafu kwa sababumakosa yetu; alitufanya tuwe hai pamoja na Kristo – yaani, tumeokolewa kwa neema. Akatufufua pamoja naye na kutuweka pamoja naye katika nafasi za mbinguni katika Kristo Yesu; ili katika nyakati zijazo audhihirishe wingi wa neema yake upitao kiasi katika Kristo Yesu” (Waefeso 2:4-7).

Paulo alikuwa akiandikia Waefeso kutoka gerezani huko Roma. Timotheo kama kijana alikuwa mchungaji wa kanisa huko Efeso, ambalo lilikuwa likikua sana na kufurahia baraka tele. Kanisa lilikuwa na hamu ya kusikia kile Paulo alichokiambia. Anaanza barua kwa kusema juu ya utukufu na ukubwa wa Kristo na kisha anawakumbusha kuhusu walikotokea. Walikuwa wamekufa kwa makosa yao na walikuwa wamepatikana hai na wamekaa katika sehemu za mbinguni katika Kristo. Sio tu kwamba dhambi zao ziliondolewa, lakini walikuwa wamehamia kwenye ufalme ambao ulizidi utukufu wa kitu chochote walichowahi kuona. Yote kwa sababu waliokolewa na neema kupitia imani!

"Kwa kuwa sisi ni kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu ili tutende mambo mema, ambayo tokea awali Mungu aliandaa ili tuenende katika hayo" (2:10). Uwepo wa Mungu utakujengea fursa za kila aina ambazo hazina budi kutoka kwa kazi zako. Ana kitu kilichopangwa kwa ajili yako ambacho unaweza kutembea ndani yake. Sio tu kwamba yeye hukuokoa na kukupa imani, lakini pia anakuita nje na kukupa maisha ya utukufu, nguvu na neema!

Kristo hauchukui ubaya kutoka kwako; anaweka ufalme wote wa utukufu wa Kristo Yesu ndani yako. Damu yake haikuoshi tu kutoka kwa dhambi, lakini huanza kuingizwa katika maisha yako ili haki ya Mungu katika Kristo ikae ndani yako. Kwa sababu ya hii, unaweza kutembea kwa ushindi na kichwa chako kikiwa wima juu.

Tags