<?xml version="1.0" encoding="utf-8"?>
<rss version="2.0" xml:base="http://www.worldchallenge.org" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/">
<channel>
 <title>World Challenge Pulpit Series Newsletters</title>
 <link>http://www.worldchallenge.org/sw/pulpit_series_newsletters</link>
 <description>Publications from the World Challenge Pulpit Series Newsletters</description>
 <language>sw</language>
<item>
 <title>Mungu Hatawahi Kamwe Kuwaacha Watu Wake</title>
 <link>http://www.worldchallenge.org/sw/node/7522</link>
 <description>&lt;p&gt;Kwa kuwa BWANA huwapenda wenye haki naye hatawaacha waaminifu wake. Watalindwa milele, lakini uzao wa waovu utakatiliwa mbali, &lt;cite&gt;(Zaburi 37: 28)&lt;/cite&gt;.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Katika kitabu cha Luka 22, Yesu atoa Onyo kali sana kwa mfuasi wake mkuu. Yesu alimwita Mtume Petero kando na kumueleza kinaga ubaga: ““Simoni, Simoni, sikiliza, Shetani ameomba kuwapepeta ninyi wote kama ngano. Lakini nimekuombea wewe Simoni ili imani yako isishindwe…” &lt;cite&gt;(Luka 22: 31 – 32)&lt;/cite&gt;.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Wakristo wachache watashangazwa na hilo jambo, kwamba Shetani alitaka kumtia Petero majaribuni. Tunajua, Petero alikuwa mkuu wa Mitume. Kwa wasomi wa Biblia, si ajabu Shetani kuomba ruhusa ya kuja kinyume na huyu Mtume jasiri. Biblia ina nakili wazi kuwa azma ya Shetani ni kuvunja Imani ya wale wamtumikiao Yesu. Kwa wale Mitume kumi na wawili, Petero ajitokeza wazi kama Yule angeweza kutetea Imani yake ndani ya Kristo.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Walakini, kuna jambo kwa hili nano linalotatanisha wakristo. Ni hili: &lt;em&gt;Mungu alimruhusu Shetani kumjaribu Petero!&lt;/em&gt; Ndio, Mungu wetu wa Mbinguni alimkubalia Shetani kumsumbua mtumishi wake wa dhamana.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Fikiria haya: Yesu alikwisha sema, Juu ya Maneno ya Petero aliyotamka kwa Imani, atalijenga Kanisa lake. Na sasa, Kristo aliweka Neno lake taabani kwa kumuweka Petero ndani ya miale ya Shetani. Tunajua, hata ingawa Petero alikuwa jasiri, alikuwa na kasoro pia.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Je, Petero angelianguka mtihani huu? Kristo angelijenga vipi Kanisa lake juu ya Maneno ya yule atetemeshwaye na Shetani? Zaidi ya hayo, ingelikuwaje Mungu mpenzi amuelekeze mpendwa wake kwa majaribu kama haya? Wakristo watatanishwa na mambo haya.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Kwa waumini wengine, jambo hili kumhusu Mungu Baba halieleweki.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Kwa wengine Kanisani, jambo hili ni zito sana kujaribu kulinganisha na Mungu. Walakini, Biblia inatueleza kuwa yaliompata Petero yamekwisha wapata wengi wapendwa wa Mungu.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Tuchukuwe mfano wa Ayubu, tafakari yale mwenye Haki Ayubu aliyopitia: kupoteza mali yake, nyumba, na hata watoto wake wa dhamana. Ndio maana Ayubu alipopitia mambo haya, wenzake wampendao Mungu walishangaa. Hawange kubali kuwa Mungu angelimruhusu Shetani kumtia majaribuni muumini wake. Katika mawazo yao, Ayubu lazima alikuwa ametenda mambo maovu yaliyomletea mikasa.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Lakini, Hakuna lile lisilo mbali na Ukweli! Katika Mlango wa kwanza wa kitabu cha Ayubu, Shetani aliingia Mbinguni kuomba ruhusa ya kumtia Ayubu katika majaribu. Mungu alimkubalia! Alimpa Shetani ruhusa kumtia mwanadamu mwenye haki katika majaribu makali mno yaliomsukuma mpaka mipakani mwa Imani yake.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Wapendwa, katika kila jambo, Biblia inanakili waziwazi: Njia moja tu ambayo Shetani hupata kujaribu Imani ya wana wa Mungu – hata Ayubu na Petero – ni kupitia ruhusa apatayo kutoka kwa Mungu Baba. Naye Mungu hageuki, Neno lake ni lile lile jana, leo na hata milele &lt;cite&gt;(soma Waibrania 13:8)&lt;/cite&gt;. Kwa hivyo, tunaweza kuwa na hakika kuwa kama vile ilivyowatendekea wale wapendwa, itamtendekea yeyote Yule anayekiri kumfuata Yesu.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Lakini hebu tazameni, Ukweli huu: Shetani hawezi kutikisa Imani ya mtoto wa Mungu bila ruhusa kutoka Mungu mwenyewe. Neno hili llinatuambia nini? Kwa ufupi: &lt;em&gt;Mungu ana sababu mwafaka na mpango maalum kwa majaribu yote ya Shetani maishani mwetu.&lt;/em&gt;&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Na kweli, Yesu alipomuonya Petero, Alimtia moyo kwa maneno haya ya ajabu: “...nimekuombea… ili imani yako isishindwe” &lt;cite&gt;(Luka 22:32)&lt;/cite&gt;. Kwa wazi, Kristo alijua Petero atashinda majaribu haya, Imani yake ikisimama Imara. Ili laamanisha kuwa, Yesu alikuwa na mpango mwafaka na Maisha ya Petero, kupitia majaribu hayo.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Mambo haya ni kweli kwetu, Yesu ameahidi kuombea Wafuasi wake, sio Petero tu lakini wote wale wanao mfuata katika vizazi vyote. Bwana wetu yuko na mpango kwa kila jaribu tupatalo.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Tafakari maonyo ya Krisot katika maandiko.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Ufunuo unatuambia kuwa Shetani amekuja chini duniani nyakati hizi za mwisho, kwa hasira kwa kuwa siku zake ni chache. Kwa sasa yuko vitani na wateule: “Lakini ole wenu nchi na bahari, kwa maana huyo Shetani ameshuka kwenu, akiwa amejaa ghadhabu, kwa sababu anajua ya kuwa muda wake ni mfupi!’&lt;cite&gt;(Ufunuo 12:12)&lt;/cite&gt;.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Tunaambiwa kuwa adui wetu Shetani anzurura kama Simba, akitaka kumeza: “Mwe na kiasi na kukesha, maana adui yenu Ibilisi, kama simba angurumaye huzungukazunguka akitafuta mtu ili apate kummeza” &lt;cite&gt;(Petero wa kwanza 5:8)&lt;/cite&gt;. Kwa ufupi, njama ya Shetani ni kula na kumeza Imani ya Wateule wa Mungu.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Pia, tunaelezewa kuwa Shetani huja kama mwizi kwa wale wanao amini: “Mwivi huja ili aibe, kuua na kuangamiza. &lt;cite&gt;(Johana 10:10)&lt;/cite&gt;. Mwizi kama huyu haibi tu bali anavunja na kumaliza kabisa Imani ya watu.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Mwishowe, tunaelezewa kuwa Shetani huleta gharika kwa watu wa Mungu, akitamani kufagia Imani yao kupitia Uoga mkuu na vita vikali: “Ndipo lile joka likamwaga maji kama mto kutoka kinywani mwake, ili kumfikia huyo mwanamke na kumkumba kama mafuriko” &lt;cite&gt;(Ufunuo 12:15)&lt;/cite&gt;.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Mambo haya yanashutua mno. Kwa wazi, Petero aliitaji maombi ya Yesu ili Imani yake iweze kusimama imara. Walakini, ni kana kwamba Petero alikuwapuuza haya.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Kwa Ujasiri wake, Petero aliamini kuwa Imani yake itastahimili majaribu ya Shetani.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Wakrsito wengi hukumbuka majivuno ya Petero kuhusu Imani yake: “Petro akajibu, “Bwana, niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani na hata kifoni.” &lt;cite&gt;(Luka 22:33)&lt;/cite&gt;. Yale anenayo Petero kiujasiri yanaweza kuonenakana kama Ujasiri wa Kiroho. Lakini, kwa kweli, inalinganishwa na Ujasiri wa kimwili tu, ndio maana Paulo akalionya Kanisa: “Hivyo, yeye ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke.” &lt;cite&gt;(Wakorintho wa kwanza 10:12)&lt;/cite&gt;.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Paulo asema, ni lazima tuwe wanyenyekevu katika vita vya Kiroho. Yuda anakili haya alipoandika: “Lakini hata Malaika Mkuu Mikaeli alipokuwa anashindana na ibilisi juu ya mwili wa Mose, hakuthubutu kumlaumu, bali alimwambia, “Bwana na akukemee!” &lt;cite&gt;(Yuda 1:9)&lt;/cite&gt;. Neno la Mungu li wazi kuhusu umuhimu wa Kunyenyekea.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Hata hivyo, wakristo wengi husahau. Nishawahi kusikia waumini wakisema, “Niko tayari kutoa maisha yangu. Haijalishi nitapitia nini. Niko tayari kufa kwa ajili ya Bwana wangu.” Petero alijivunia vivyo hivyo. Lakini saa ilipofika, hakuwa tayari. Pale Petero alipokumbwa na nafasi nzuri ya kufa kwa ajili ya Kristo, alifanya jambo ambalo hakuwahi kudhania hapo mbeleni. &lt;em&gt;Alimkana Bwana Yesu.&lt;/em&gt;&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Katikati ya vita, pale Petero angelikiri Imani yake ndani ya Krsito, alilaani. Katika giza la uoga na dhiki, Mtume huyu alinena mbele ya wote pale, “Sikuwahi kumjua Mtu huyu!” jameni ni wakati mgumu vipi ulikuwa kwa Petero? Mjasiri mkuu wa waumini alishushwa mpaka kuwa muoga, akiogopea maisha yake.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Ninahakika ya kuwa, wakristo wengi huamini kuwa hawawezi kutenda dhambi kama hii ya Petero. Wao hujiambia, wako juu ya dhambi kama hii. Wanajiona wakimfuata Yesu mpaka kufa. Nina Jambo muhimu la kuwaambia waumini hawa: hakuna mkristo yeyote anayeishi leo aliye juu ya makosa ya Ayubu au Petero. Pale majribu makali yanapotujia kutoka kwa muovu, kama vile yalivyo wakumba watu hawa, sote hukumbwa na mkasa wa kutikiswa kwa Imani.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Sitaki kumshtua yeyote Yule, kwa matamshi yangu kuwa sote tunaweza kuanguka.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Nataka tu nisisitize hili kwa kuwa ni jambo muhimu mno. Biblia iwazi, nami nawaona waumini wengi walio karibu kukata tama.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Mimi najmjua Mtumishi mmoja mpendwa ambaye Imani yake imetikiswa. Ninaongea kuhusu waume na wake wa Imani kuu. Wale wanao Ubiri na kutenda uponyaji na miujiza. Hawa ni Wateule ambao singefikiri ya kuwa wangemshuku au kukosa kumuamini Mungu. Nilikuwa na hakika, “kama kuna Yule awezaye kupitia gharika, tazama huyu ni Mtumishi wa Mungu awezaye hayo!”&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Lakini, waumini wengine sasa wanashuku hata kama Mungu kweli hujibu Maombi. Wakati mmoja Imani yao ilikuwa kuu iliimarisha Imani ya wengine. Lakini sasa, kama Ayubu na Petero, majaribu makali yamewakumba, wamejikuta katika vita wasivyoweza kustahimili, na wameanza kulegea.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Pale Petero alipokuwa katikati ya vita hivi, Yesu alikuwa akimuombea. Jameni, kwangu mimi, hili ndilo Neno la kutia moyo sana ndani ya Biblia yote: “Lakini nimekuombea wewe Simoni ili imani yako isishindwe,” &lt;cite&gt;(Luka 22:32)&lt;/cite&gt;. Tafakari yale Yesu alikuwa anamueleza Petero. Alimhakikishia kuwa, lolote atakalo pitia, - haijalishi ni jambo gani hilo, hata kama ni kumkana Krsito – &lt;em&gt;Imani yake Haitazimia.&lt;/em&gt;&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Kwa kweli, Petero hakuwa ameachwa na Mungu – ata kwa dakika moja. Hakuachwa ata alipo mkana Kristo na kutoroka. Yule aliyekuwa Jasiri, sasa alivunjika kwa makosa yake, hakuwahi kuwa pekee hata kidogo. Wapendwa nasi pia ni vivyo hivyo.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Haijalishi majaribu yanayokukumba – iwe ni uchungu gani unayopitia, jaribu unalopitia, makosa gani unayowaza.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Wakati huu – katikati ya gharika, uchungu na majonzi – Yesu anakuombea. Anakupigania. Na hajawahi kukuacha peke yako.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Tafakari neno la kutia moyo; Yesu alimueleza Petero, pamoja na Onyo. “nawe ukiisha kunirudia, uwaimarishe ndugu zako.” &lt;cite&gt;(Luka 22:32)&lt;/cite&gt;. Neno hili laja pale tu Yesu alipomueleza Petero kuwa atapepetwa, kwa kweli, maneno haya yote yako katika mstari mmoja!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Wapendwa, hili ndilo himizo la kutia moyo kwetu sote. &lt;em&gt;Mungu muumba ametushikilia mikononi mwake.&lt;/em&gt; Anatueleza, kama vile Petero, “Amka, nenda sasa. Usibaki kwa makosa yako. Bali, enenda ukawalishe kondoo wangu. Nenda ukawaonya wapendwa wangu kuhusu mbinu za muovu dhidi yao. Waeleze nimewashikilia kwa mikono yangu, katika majaribu yote.”&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Kwa ufupi, Petero alikuwa na kazi muhimu ya kufanya. Na alikuwa na ujuzi mkuu kuhusu Neno alilopaswa kuhubiri. Jua kwamba, Yesu aliambia Kanisa kuwa hatuweza kutojua au kupuuza mbinu za Shetani. Petero angeliweza basi kuwaeleza waumini, sio tu majaribu watakayopitia, lakini pia vile Mungu muaminifu atawaokoa kutoka hata kwa majaribu makuu.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Lazima tujuwe kwa hakika mbinu na mipango ya adui. Na silaha kuu zaidi anatumia Shetani ni Uongo – Uongo mkali kinyume nasi, kutoka kwa mdomo wa baba wa Uongo! Uongo wake mkuu ni upi? &lt;em&gt;Kwamba Mungu si muaminifu kwa watu wake.&lt;/em&gt;&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Kama vile alivyo fanya tangia jadi, Shetani huomba ruhusa kutoka kwa Mungu atupepete leo. Anataka kupiga Nyumba zetu, Ndoa zetu, Watoto wetu, Afya zetu, Kazi zetu, Ujuzi wetu, na Imani yetu ndani ya Bwana. Hii ndio gharika ambayo Ufunuo unanena: Gharika ya majaribu kinyume na Imani yetu.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Unaweza labda kushangaa: “Kunaweza kuwa kubaya kiasi gani kwa Muumini? Mungu hurusu mpaka wapi anapo kubali tupepetwe? Nitawaelekeza kwa Waibrania 11, pale tunasoma majaribu yaliowakumba wajasiri wa Imani. Neno lasmea, “Hawa wote walishuhudiwa vema kwa sababu ya imani yao” &lt;cite&gt;(Waibrania 11:39)&lt;/cite&gt;.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Masumbuko waliopitia hawa majasiri wa Imani, ndio yale tunayopitia hata leo.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Natafakari Wakristo walio kule Iraki, wanaopitia mambo yakushtua Imani yao katikati ya vita. Wengi wao iliwabidi watoroke kuokoa maisha yao, wakiacha nyuma nyumba zao, kazi na Kanisa. Ili wanusurike, ilibidi wakimbie Asiria, Yordani na miji ya kando ambayo pia hayana urafiki na Wakristo. Hawa waumini kutoka Iraki hawana kazi wala makao, hawana pa kutorokea. Lazima waombe kila siku kupata chakula. Wengi wameuawa. Hata hivyo, wanaendelea kuubiri Injili katika nchi hizi za ukimbizi pale wametorokea kwa sababu ya vita.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Nimekwisha pata habari kutoka wa waumini hawa kutoka Iraki. Wameandika, “Ndugu David, Majaribu si eti yanakuja, kwetu sisi, majaribu makali yamekuwa nasi kwa miaka mingi sasa.” Wameona taabu tangu jadi, wameelewa kukwamilia Imani. Kama Petero, wametengwa Kuubiri na nguvu, wakilionya Kanisa la Kristo.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Mimi naamini kwa kweli, wengi wetu tuko katika majaribu makali kutoka kuzimu, tunastahimili majaribu ya kishetani. Je wewe? Kama hujapatwa na jaribu la Imani? Ninakusihi: shukuru Mungu. Lakini, nyenyekea, usiwahi kujisifu kuwa Imani yako ni ya nguvu kuliko wengine.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Shetani hungojea mpaka pale anayejaribiwa amevunjika moyo, na kuisha nguvu. Yeye hungoja mpaka pale maombi yana kaa kana kwamba hayajibiwi – pale matumaini yamekwisha kabisa, pale ambapo mbinu zetu zimekwisha. Hilo ndilo lilimtendekea Petero, alipomuona Bwana wake akiteswa mbele ya kikao cha Mafarisayo. Iilimtendekea Ayubu, aliye lazimika kuwaza alipo poteza kila kitu cha muhimu kwake.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Maswali yanapochipuka akilini mwa anaye pitia majaribu – “Mungu, ukowapi? Kwanini maombi yangu hayajibiwi?” – papo ndipo Shetani huchagua kupanda Uongo wake: “Mungu amekuacha. Amejitenga nawe. Hakusikii.”&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Kumbe Mungu hajakuacha – na hatawahi kukuacha. Kwa kweli, sasa hivi anakuambia hivi: “nimekuhakikishia sitakuacha kamwe. Sasa basi, simama, enenda ukalishe kondoo wangu. Chunga mbinu za Shetani kinyume nawe, tazama, niko nawe, hata mpaka mwisho wa Dunia.” Amina!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;(Maandiko yamenakiliwa kutoka kwa IBS-STL Global translation http://www.ibs.org/bibles/swahili/index.php)&lt;/p&gt;</description>
 <category domain="http://www.worldchallenge.org/sw/taxonomy/term/275">David Wilkerson</category>
 <pubDate>Fri, 22 Jan 2010 15:14:35 -0600</pubDate>
 <dc:creator>thomas_rewe</dc:creator>
 <guid isPermaLink="false">7522 at http://www.worldchallenge.org</guid>
</item>
<item>
 <title>Najua Kwa Hakika</title>
 <link>http://www.worldchallenge.org/sw/node/6850</link>
 <description>&lt;p&gt;“Ninamjua Yeye niliyemwamini na kusadiki ya kuwa anaweza kukilinda kile nilichokiweka amana Kwake hadi siku ile. (Timotheo wa Pili 1:12, my italics). Haya ni maneno ya mtu aliyekuwa mwisho wa maisha yake, Mtume Paulo alikuwa akimueleza mwanafunzi wake, Mtumishi mchanga aliyekuwa mafunzoni, Timotheo. Katika barua hii, Paulo alimnong’onezea Timotheo maneno haya mazito. “Nimevipiga vita vizuri, mashindano nimeyamaliza, imani nimelinda” (Timotheo wa Pili 4:7). Ingawa Paulo aliamuandikia Timotheo, maneno haya yana umuhimu kwa kila Mkristo anaye pitia mateso. Tafakari: wakati huu wa majaribu – alipokuwa kifoni – Paulo alikua na hakika kamili kuhusu Upendo wa Mungu kwake. Na tena, aliamini kabisa uwezo wa Bwana Mungu “kukilinda kile nilichokiweka amana Kwake” ingawa ushahidi wote ulikuwa kinyume na mawazo haya.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Wapendwa, Mawaidha ya Paulo ni yetu sote tulio kumbwa na vita vya kiroho, tunao pitia shida kama majeshi wazuri. Paulo angewezaje kuongea kuhusu uaminifu wa Bwana katika majaribu? Ni nini haswa alichokuwa na hakika nacho kumhusu Bwana Mungu iliyo zaa Imani kiasi hiki? Paulo hakusema ni nini “alichokiweka amana Kwake (Mungu) hadi siku ile”. Tunaweza tu kubahatisha ni nini haswa alichomkabidhi. Walakini, kama Paulo, nasi inatubidi tuwe na Hakika kamili katika Imani kwamba Bwana Mungu anaweza kuviweka vile tulivyo mkabidhi. Kukumbana na majaribu ya nyakati hizi, inatubudi tuwe na hakika kamili kuhusu Mungu wetu.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;1. Lazima Tuwe Na Hakika Kwamba Hakuna Kile Kinachoweza Kututenganisha Na Upendo Wa Mungu Ndani Ya Yesu Kristo.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Paulo aliandikia Warumi:&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;“Kwa maana nimekwisha kujua kwa hakika ya kuwa wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuja, wala wenye uwezo, wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kingine cho chote kitakachoweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.” (Warumi 8:38–39). Kabla ya kutoa Tamko hilo, Paulo aliuliza swali: “Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je, ni shida au taabu au mateso au njaa au uchi au hatari au upanga?...Lakini katika mambo haya yote tunashinda, naam na zaidi ya kushinda, kwa Yeye aliyetupenda” (Warui 8:35, 37). Ni wazi kwamba Paulo kupitia maswali haya anaonesha kuelewa makusudi ya Shetani siku hizi za Mwisho: Kuzuia watoto wa Mungu kutembea katika Upendo wa ajabu. Lakuhuzunisha ni kwamba, maelfu ya wale walio Kanisani ni vipofu kwa mitego ya muovu. Wengi wanaishi wakiwa hawana habari kuwa wamefungiwa kujua na kufurahia Upendo wa Mungu kwao.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Usinielewe vibaya, hatufaye kamwe kumuogopa yule Muovu. Lakini kama hatuelewa mbinu zake za kupingana na Imani yetu, tutaendelea kushindwa maishani. Paulo alijua umuhimu wa kuziweka wazi mbinu za Shetani. Tunapoweza kuzifahamu hizo mbinu zinazopinga Imani yetu, ndiposa twaweza kusema kama Paulo, “Ninaamini kua - hakuna uongo wala mashtaka – yataweza kunitenganisha na Upendo wa Mungu, iliyo ndani ya Yesu Tristo.” Lazima tuelewe kua Shetani ana nia ya kufunga kila huduma inayo ongozwa na Roho Mtakatifu, kuwashurutisha Wakristo wakiroho siku hiz za Mwisho. Analenga kila Muumuni aliye simama imara kupingana na ufamle wa giza, sio tu wachungaji.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Miaka michache sasa nimekuwa na msukumo moyoni kwamba masaibu ya wateule wa Mungu siku za leo hayajawahi kuonekana katika historia ya Kanisa la Tristo. Wateule wa Mungu wamekuwa wakipitia masaibu mengi. Waibrania 11 inaeleza haya. Na sasa, Neno linasema, Shetani ameinuka kinyume na Kanisa kwa sababu wakati wake ni mfupi. “Kwa hiyo, furahini ninyi mbingu na wote wakaao humo! Lakini ole wenu nchi na bahari, kwa maana huyo Shetani ameshuka kwenu, akiwa amejaa ghadhabu, kwa sababu anajua ya kuwa muda wake ni mfupi!’ (Ufunuo 12:12). Kurudi kwake Yesu uko Mlangoni, akiwa na hasira nyingi, Muovu na adui wa Nafsi zetu amekuja kudanganya hata Wateule wa Mungu. Hata sasa, majeshi ya watumishi wa Shetani yanaendelea kuvunja moyo na kuwaaharibu wateule wa Mungu. Paulo atoa ushuhuda kuhusu mateso aliopitia maishani akisema, “Maana tulitaka kuja kwenu, hasa mimi Paulo, nilitaka kuja tena na tena, lakini Shetani akatuzuia. (Wathesalonike wa Kwanza 2:18).&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Katika Karne iliyopita, T. Austin Sparks aliandika kuhusu vita vya Shetani siku hizi za Mwisho. Mtumishi huyu wa Mungu aliona mambo mengi yakizuiwa, yakishindikizwa chini, yakibanwa na Shetani, kana kwamba maelfu ya Wakristo wameshindwa kutekeleza huduma zao….kwa sababu ya Uzuizi wa Shetani. Kama Paulo hapo mbeleni, Austin-Sparks alionya watu wa Mungu wawe makini kwa mbinu za Shetani. Aliwasihi waumini waombe kumsihi Mungu amshushe Shetani kutoka pale mahali ambapo “anawashtaki waumini”. Ninaamini Maombezi kama hayo ni ya kweli kwa Muumini yeyote alione Uzuizi wa Shetani. Waumini hawa wanajua kamili vita inayowakumba wale wanao ongoza wengi katika njia safi ya Kristo.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Nimekuja Kuamini Kwamba Lengo Kuu La Shetani Ni Kuzuia Waombezi Wa Mungu.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Nini basi maana ya Muombezi? Huyu ni yule ambaye hubeba mizigo ya wengine kwa Maombi. Mtumishi kama huyo hachoki Kuombea Kanisa la Kristo au yeyote yule Bwana ameweka kwa Roho yake. Enzi zote, Mungu ameweka Waombezi mbele ya Vita, kufanya vita kinyume na nguvu za giza. Waombezi hawa leo wanapatikana katika nchi zote duniani. Kuna sababu wanaitwa “Majeshi ya Waombezi”. Wengi wanaotuandikia wanaeleza vita katika Maisha yao wenyewe. Muombezi aliye na miaka 91 alisema haya: “nasikia kuisha nguvu, baada ya utumishi wangu wa miaka mingi kwa Mungu nikipigana kila aina ya vita. Niko mnyonge mwilini baada ya Miaka mingi ya shida – nikishughulikia shida na masaibu ya wengine….tangu nilipokuwa miaka 4, nimewapenda na kuombea wengine. Nimekuwa Muombezi miaka hii yote….ninaichukua na kurejeshi umilki wangu kila mara Shetani anajaribu kuiba, kwa kuomba kiroho… na ninapokea nguvu mpya.” Maisha yote, mtumishi huyu alichukulia maanani mawaidha ya Yuda: “Lakini ninyi wapenzi, jijengeni katika imani yenu iliyo takatifu sana tena ombeni katika Roho Mtakatifu. Jilindeni katika upendo wa Mungu mkitazamia kwa furaha rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo ili awalete katika uzima wa milele.” (Yuda 20 – 21). Ujumbe kwa wale wale wapiganao vita vya kiroho ni wazi: Jijengeni katika imani yenu. Jilindeni katika upendo wa Mungu. Tafakari kwamba Yuda atia nguvu Ujumbe wake kwa kutusihi tuombe katika Roho Mtakatifu. Haiwezekani kamwe kujenga Imani kupitia nguvu au uweza wa kimwili. Bila Roho Mtakatifu, hatuweza kuwa kamili katika ufahamu wa upendo wa Mungu kwetu. Hatuweza kukabidhi nguvu za giza pekee yetu. Hatuweza hata kuinua ngao za Imani kuzima mioto ya kuzimu kwa kujaribu kuelekeza akili zetu. Tuna muhitaji Roho wa Mungu anaye tuweka Nguvu katika kila hali.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Nyakati hizi za shida, kunakili Neno pekee haitoshi. Najua mtumishi ambaye ufahamu wake katika Neno la Mungu lilikuwa maradufu aliitwa “Biblia inayotembea.” Mtu huyu angeweza kunakili vitabu vizima kutoka kwa Bibilia. Alipokumbwa na masaibu makuu, alianguka katika Imani. Kama Paulo anavyo nena, “kwa kuwa andiko huua bali Roho hutia uzima. (Wakorintho wa Pili 3:6). Ni huzuni kwamba wakristo wengi wanaokiri kujazwa na Roho hawamrudii Roho Mtakatifu wanakumbwa na shida. Hawaelewi Amani na Utulivu wake, wakati kazi yake kuu ni kutupatia vitu hivi. Waumini hawa bado hawajajua kumtegemea Roho, labda ni kwa sababu hawajajua kwa hakika kuwa wanamuhitaji.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Shida Ni Kwamba Wakristo Wengi Hupanga Kama Ngazi Ule Utatu Wa Mungu. Tukijieleza Kwamaba Mungu Baba Ndio Mkuu, Kisha Yesu Alafu Roho Mtakatifu Akiwa Wa Watatu.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Ukweli ni kwamba Roho Mtakatifu ni Mungu, anayepasa kuabudiwa na kuheshimiwa. Baada ya miaka 20 ya huduma, nimeafikia jambo hili; umuhimu wa Roho Mtakatifu katika maisha yetu. Kwa ufupi, nimeweza kuelewa, kutomuombea muumini yeyote kabla ya kumuita Roho Mtakatifu avunje vikwazo vyote kutoka kwa Shetani. Kila muumini lazima ajuwe pingamizi za Shetani kinyume na Ahadi za Mungu. Baada ya kumuita Roho Mtakatifu ndiposa naweza kuomba na yeyote yule ili Roho Mtakatifu afunguwe moyo wake aweze kupokea Upendo wa Mungu. Ningeliweza kunakili Neno chungu nzima, naweza kumuhurumia katika shida zake, na kufanya yote kuinuwa Roho yake. Lakini ni lazima yeye mwenyewe ajuwe Upendo na Amani ambayo Roho Mtakatifu pekee anaweza kumpatia.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;2. Lazima Tuwe Na Hakika Kamili Kuwa Mungu Hu Bariki Wale Wamchao Bila Kusita.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;“Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu, kwa maana ye yote anayemjia Mungu lazima aamini kwamba Yeye yuko na ya kuwa huwapa thawabu wale wamtafutao kwa bidii.” (Waibrania 11:6). Mara nyingi tunasumbuka kushikilia Imani. Sote tunatamani Ahadi za Mungu, si kwa Amani yetu pekee lakini pia kumpendeza Mungu. Tunatamani Imani imtukuzayo Mungu. Kwa sababu hii, tunapata kusononeka maombi yetu yasipojibiwa. Tuanaanza kushuku Imani yetu, tukishangaa “je, uaminifu wangu kwa Mungu ni nadra sana? Je, niko mnyonge kuamini? Kwa nini mbingu zimefungwa juu yangu? Je, nimekwepa njia kidogo? Je, sija makinika ya kutosha? Je, kuna mizizi ya kutoamini ndani yangu? Tunajaribu sana kuamini, tuking’ang’ana kumpendeza Mungu na Imani kuu, mpaka tunazima Imani yetu kwa sababu ya hukumu tunayojitweka. Sasa, baada ya miaka 60 nikiwa katika huduma ya Mungu, nataka kuwaeleza Imani ya kamili ni nini kwangu:&lt;/p&gt;
&lt;ul&gt;
&lt;li&gt;Ni, kushikilia kamili Ahadi za Mungu pale ambapo hakuna kielelezo chochote kinachoonesha kutekelezwa kwa Ahadi hizo.&lt;/li&gt;
&lt;li&gt;Ni, kumuamini Roho Mtakatifu kwa Utulivu wa Nafsi yangu, ni kiwa na hakika kwamba Mungu anayatenda yote na lengo la kunipatia mema&lt;/li&gt;
&lt;li&gt;Ni, kukwamilia Ujumbe wa Paulo: “Nasi tunajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hutenda kazi pamoja na wote wampendao, katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi Lake. (Warumi 8:28).&lt;/li&gt;
&lt;/ul&gt;
&lt;p&gt;Ujumbe maarufu wa Paulo kuhusu “katika mambo yote Mungu hutenda kazi pamoja kwa mema” litajaribu Imani yetu tena na tena maisha yetu yote. Mara nyingi kwa macho ya kimwili, mambo yetu yanakaa kana kwamba yametumbukia nyongo. Walakini, katika majaribu yote, kuna kazi ya kweli ya milele inayoendelea pale. Mungu ayatenda yote pamoja kwa mpango wake juu yetu. Tunajuwa ilikuwa hivyo kwa Yosefu. Alipitia masaibu tele yaliokuwa shida tupu. Mpaka mwisho “Wakati Neno la Mungu lilipokuja (Zaburi 105:19). Mpaka wakati huwo, Neno la Mungu lilimjaribu. Je, unaweza basi kusema pamoja na Yosefu na Mtume Paulo “Yote yanafanya pamoja kwa mema? Je, Nafsi yako imetulizwa na ukweli huu, kwamba Mungu anafanya yote katika mpango kwa sababu yako? Unaamini kuwa katika uchungu wako – katika shida zako – katika upungufu wa ndoto zako, matumaini na malengo – Mungu alikuwa akiboresha undani wa imani yako kwake? Kwa Upendo wake, amekuwa akikuelekeza kwa Baraka, utakayopokea sasa na hata milele!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Mungu anatueleza katika Waibrania, “ni lazima uamini mimi ndimi Mbariki wako” tena muandishi asema, “Inawapasa kuvumilia ili mkiisha kufanya mapenzi ya Mungu mpate kile alichoahidi. (Waibrania 10:36).&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Mungu haja Ahidi zaidi ya yale anayotaka kufanya. Abrahamu aliweza kuelewa haya tangu mwanzo wa Imani yake. Paulo asema, “Lakini Abrahamu hakusitasita kwa kutokuamini ahadi ya Mungu, bali alitiwa nguvu katika imani yake na kumpa Mungu utukufu, akiwa na hakika kabisa kwamba Mungu alikuwa na uwezo wa kutimiza lile aliloahidi. (Warumi 4:20–21).&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Kwa Imani, Abrahamu “Alimtukuza Mungu”&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Kama Abrahamu, tunamtukuza Mungu tunapoamini Ahadi zake zote. Pale mambo yote yanapokuwa sawa, ni rahisi kuwa na ushuhuda, “Mungu aweza kutenda yote!” tunaweza kueleza wengine kwamba Mungu atajibu maombi yao. Tunaweza kunena kuwa Mungu hutimiza Neno lake. Lakini mambo yanapoenda mrama kinyume na Ahadi za Mungu – pale vielelezo vyote vinakaa kama hukumu wala sio baraka – Roho Mtakatifu huinuka akiwa na Maneno halisi ya kutuliza. “Shikilia. Muamini! Hujatengwa na Upendo wa Mungu. Yuko kazini kila dakika ya Imani yako. Usitingisike. Bali, inuka na pigana vita vizuri vya Imani”&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Nitawaaga na ujumbe huu maradufu kutoka kwa mtume Paulo. Anayetukumbusha Uaminifu wa Mungu katika kila hali, kila dakika ya maisha yetu.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;“Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je, ni shida au taabu au mateso au njaa au uchi au hatari au upanga? Kama ilivyoandikwa : ‘‘Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa, tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.’’ Lakini katika mambo haya yote tunashinda, naam na zaidi ya kushinda, kwa Yeye aliyetupenda. 38Kwa maana nimekwisha kujua kwa hakika ya kuwa wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuja, wala wenye uwezo, 39wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kingine cho chote kitakachoweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.” (Warumi 8:35–39).&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Amina!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Maandiko yamenakiliwa kutoka kwa IBS-STL Global translation http://www.ibs.org/bibles/swahili/index.php)&lt;/p&gt;</description>
 <category domain="http://www.worldchallenge.org/sw/taxonomy/term/275">David Wilkerson</category>
 <pubDate>Wed, 27 May 2009 16:36:15 -0500</pubDate>
 <dc:creator>thomas_rewe</dc:creator>
 <guid isPermaLink="false">6850 at http://www.worldchallenge.org</guid>
</item>
<item>
 <title>Maneno ya Kutuliza Yenye Matumaini</title>
 <link>http://www.worldchallenge.org/sw/node/6425</link>
 <description>&lt;p&gt;Yesu alikuwa akihutubia umati mkuu pale ambapo watu walianza kuwa na njaa. Alimtwaa mtume Filipo na kumuuliza swali muhimu. “Yesu alipotazama na kuuona ule umati mkubwa wa watu ukimjia, akamwambia Filipo, “Tutanunua wapi mikate ili watu hawa wale?” Aliuliza swali hili kumpima, kwa maana alishajua la kufanya (Yohana 6:5–6). Yesu alikuwa akisema, “Filipo, maelfu ya watu wana njaa. Niambie, tutawalisha namna gani? tufanye nini?” Jameni ni mapenzi ya aina gani kutoka kwa Kristo. Alikuwa anajua lakufanya; biblia inatueleza hivyo. Alikuwa anamfunza Filipo jambo muhimu. Funzo hilo lina umuhimu sana kwetu haswa nyakati hizi tulizoko. Wakati huu Dunia inatikiswa kushinda nyakati zingine zote katika historia. Misukosuko hii imekuja pale Wakristo kote duniani wanapitia majaribu makuu. Maelfu wamekaa usiku mzima wakijaribu kuwaza shida zao. “Labda hili litafanya kazi – hapana, hapana. Labda hili ndilo suluhisho – hapana, hilo halitafanya kazi. Nitafanya nini?” Yesu alipomuuliza Filipo hilo Swali, Wafuasi hawakuwa tu na shida ya mkate. Walikuwa na shida ya mtambo wa kutengeneza mkate, shida ya pesa, shida ya kutawanya, shida ya usafiri na shida ya masaa. Ukiunganisha kila kitu, walikuwa katika shida ambayo wao wenyewe hawangeliweza kudhania. Walikumbwa na jambo lisilowezekana.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Wapendwa, tafakari haya: ni katikati ya janga lako kuu, Yesu akaja na kukuuliza, “tutafanya nini kuhusu jambo hili?” Anajua kamili lile atakalofanya. Yuko na mpango. Lakini angependa kujua tu vile wewe ungelifanya. Jibu sawa kutoka kwa Filipo lingekuwa, “Yesu, wewe ni Mungu. Hakuna husiloweza kufanya, kwa hivyo nimekukabidhi shida hii, sasa si shida yangu tena bali ni yako.” Kupita mambo yote, Yesu alitaka Filipo akumbuke maneno ambayo alikuwa amekwisha waeleza mbeleni kuhusu Uaminifu wa Mungu. Ninaamini Kristo angependa watu wake wote leo wawe hivyo. Ametupea maneno yenye nguvu mno, yenye kutuliza na yenye Matumaini haswa kwa nyakati kama hizi za shida. Ni sisi tijikumbushe Ukweli huu tunapopitia nyakati hizi za shida.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;1. Mungu anatukumbusha, “Mimi ni Nguvu, na wa Huruma&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;“Kisha Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia, “Ninahurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa pamoja nami kwa muda wa siku tatu na hawana cho chote cha chakula, nami sipendi kuwaaga wakiwa na njaa wasije wakazimia njiani.” Mathayo 15:32): Yesu anena Jambo kwa waumini katika vizazi vyote. Anatuambia, “Nitatenda kwa watu wangu mambo zaidi ya kuwaponya tu. Nitahakikisha wako na mikate ya kuwatosha. Ninahusika na mambo yote katika maisha yao. Nataka mujuwe kuwa mimi ni zaidi ya nguvu tu. Mimi pia ni Huruma. Ukiniona tu kama mponyaji au mtenda miujiza, utakuwa ukiniogopa tu. Lakini ukiniona mimi kama mwenye Huruma, anayepeana zawadi njema, utanipenda na utaliamini Neno langu.”&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Ninaandika habari hii kwa kila Mkristo aliyekaribu kukata tamaa, karibu kuzimia, wewe uliyekabwa na shida wakati huu. Umekuwa mtumishi muaminifu, anayelisha wengine, anayeamini kwamba Mungu anatenda yale yasiowezekana kwa sababu ya watu wake. Lakini una Tashwishi kana kwamba Mungu hashughuliki na shida zako wakati huu. Tafakari wale walio katika mwili wa Kristo ambao umekwisha wahi kubariki na maneno ya kutuliza na ya matumaini, wale waliokosa matumaini. Umewaambia, “shikilia! Mungu ni wa miujiza, na ahadi zake ni za kweli. Usikate tamaa, yeye atakujibu.” Mimi nimekwisha peana mawaidha kama hayo mara nyingi. Walakini, hapa karibuni, Roho Mtakatifu aliniuliza, David, wewe unaamini kweli miujiza? Jibu langu lilikuwa, “Ndio, Bwana, ninaamini. Ninaamini miujiza yote niliyosoma katika maandiko. Jibu hili halikutosha. Mungu anauliza waumini swali, “Je unaamini kwamba mimi naweza kukutendea miujuza yako binafsi?” na sio tu Miujiza moja, lakini katika kila Janga na katika kila hali unayopitia.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Tunahitaji zaidi ya miujiza tuliyosoma katika Maandiko. Tunahitaji miujiza yetu ya kisasa, ya kibinafsi, katika hali ambayo hatuja wahi kukumbwa nayo hapo mbeleni. Unapokabwa na hali hii ya shida, unaamini kwamba Mungu atalisuluhisha? Unaamini kwamba atatenda miujiza kwa njia ambayo hukuwahi kukusudia? Hilo ndilo Swali Yesu alimuuliza Filipo. Ni Swali linalo hitaji Imani – Imani inayotuliza Moyo na kufanya “kukomeshwa kwa vita”. Ni Imani kama hiyo itakayoweza kutufanya tutulia ndani ya Baba, tukimuamini kwamba atatujibu kwa wakati wake.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;2. “Imani Yetu wakati wa shida inatuwezesha kuwa an Ushuhuda wa “Ripoti Nzuri”&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;“Naam, kwa imani baba zetu wa kale walishuhudiwa. (Waibrania 11:2). Neno la kigiriki ninalomaanisha “Kushuhudiwa” linaweza kulinganishwa na “kuwa Ushuhuda”. “Baba zetu walikuwa na Imani iliyo kita Mizizi. Imani isiyotikisika iliyogeuka kuwa Ushuhuda duniani kuhusu Uaminifu wa Mungu wakati wa shida. Tafakari yale waliopitia hawa baba zetu: Gharika, Kutukanua, Pingu, Jela, Moto, Mateso, Vita na shimo la simba. Katika haya yote, Imani yao kwa Bwana haikutikiswa. Kwanini? Walikuwa na hakikisho la ndani kwamba Mungu alikuwa amefurahishwa nao. Baba zetu walijua Mungu amewafurahia, akisema, “Vyema! Mumeniamini.” “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu, kwa maana ye yote anayemjia Mungu lazima aamini kwamba Yeye yuko na ya kuwa huwapa thawabu wale wamtafutao kwa bidii. (Waibrania 11:6). Tunapokwamilia Imani yetu nyakati za shida, huwa tunapokea hakikisho kutoka kwa Roho Mtakatifu: “Vyema. Wewe ni Ushuhudu wa Mungu inayopendeza”&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Unapotulia ndani yake wakati wa Gharika, ukikwamilia Imani yako, unapokea “Ripoti Nzuri.” Na ndipo unakuwa ishara ya matumaini kwa wale wanaoshuhudia. Wale wanao tafakari maisha yako – nyumbani, kazini, mtaani – wanasoma kwamba Tumaini lipo hata kwao pia. Wanapokutazama vile ulivyo ndani ya shida zako, wanagundua, “pale kunasimama mtu ambaye hajapoteza Imani yake kwa Mungu. Hana uoga kamwe. Ni nini inamfanya awe wa Imani katikati ya janga? Mungu wetu amepatiana yote yanayotakikana kuimarisha Imani yetu, ata kama Janga zitaongezeka. Tumepewa Roho Mtakatifu, Anaye ishi ndani yetu na kukaa nasi, na Ufunuo wa Neno la Mungu. Yote haya yata tuimarisha, na kutuwezesha kupata Ushuhuda wa Ripoti Nzuri hata dunia inapotetemeshwa.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;3. Tumepewa silaha maradufu kupinga Uoga.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Uoga unapotukumba inabidi tukumbuke Ukuu wa Mungu wetu. Inatupasa tukumbuke Ukombozi wake kwa wale wanao muamini, na kuitisha hiyo Nguvu ya Kiungu katika shida zetu. Uoga hauwezi kumkaba Muumini anaye jua Ukuu wa Mungu. Nehemia alijua haya vyema. Alitembea huku na kule pale ambapo Yerusalemu ilikuwa imezingirwa na mataifa waliokusanyika kwa vita. Waumini Mabakio walikuwa wakifanya kazi usiku na mchana kujenga ukuta wa Yerusalemu kujikinga na maadui hawa. Ililawalazimu washike nyundo kwa mkono mmoja na panga kwa mkono wa pili. Baada ya mda, Uoga uliwaingia. Walijikinga vipi na Uoga? Nehemia aliwakumbusha Ukuu wa Mungu wao: “Baada ya kuona hali ilivyo, nilisimama na kuwaambia wakuu, maafisa na wengine wote, “Msiwaogope. Mkumbukeni Bwana, ambaye ni mkuu mwenye kuogofya, piganeni kwa ajili ya ndugu zenu, wana na binti zenu, wake zenu na nyumba zenu.’’(Nehemia 4:14).&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Hivi ndivyo Musa alikabidhi Uoga ndani ya waisraeli: “Mnaweza kujiuliza wenyewe “Mataifa haya ni yenye nguvu kuliko sisi. Tutawezaje kuwafukuza?’’ 18Lakini msiwaogope.Kumbukeni vema jinsi BWANA Mungu wenu alivyofanya kwa Farao na kwa wote huko Misri. …Msiingiwe na hofu kwa sababu yao, kwa kuwa BWANA Mungu wenu, ambaye yupo miongoni mwenu ni mkuu naye ni Mungu wa kutisha. (Kumbukumbu la torati 7:17–18, 21). Musa alikuwa anasema, “mutakutana na maadui wengi walio na nguvu kuwaliko. Mutatafakari vile ushindi utapatikana katika hali hii. Lakini, kumbukeni Ukuu wa Mungu. Jikumbusheni vile alivyowaokoa nyakati zilizopita na uaminifu wake katika ukombozi. “Yeye ni sifa yako, yeye ni Mungu wako, ambaye alikutendea yale maajabu makubwa na ya kutisha uliyoyaona kwa macho yako mwenyewe” (Kumbukumbu la torati 10:21). Kama Imani yako imetikiswa, jikumbushe Ukuu wa Mungu. Kumbuka Ukombozi wake katika Maisha yako. Utaona Uoga wote ukivunjwa na ufunuo wa Ukuu wa Mungu.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;4. Tuko na silaha ya kupinga sauti za kukata tamaa.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Katika shida zetu Leo, wengi wamepoteza Imani. Imani kuu zimegeuka na kuwa kukata tamaa. Wengi wanashangaa katika shida zao, “kwanini Mungu hajibu maombi yangu? Je, nimefanya kosa? Sielewi ni kwanini shida yangu inaendelea bila kukoma, je, Mungu amenikasirikia? Kuna wale ambao wame wasiliana nasi wakisema, “sina wakuongea naye, sina yule wakulia naye, nahitaji mtu ambaye nitaweza kumueleza moyo wangu.” Kawaida sisi tungependa to binadamu mwengine mwenye sura, macho na masikio kutusikiza na kutupea mawaidha.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Ayubu alipo lemewa na mikasa, alilia kwa uchungu, ‘‘Laiti kama angekuwapo mtu wa kunisikia!” (Ayubu 31:35). Alisema haya pale alipokuwa amezungukwa na wale waitwao marafiki, wale waliohuzunika kwa mateso yake. Kwa kweli, watu hawa walikuwa wapasha habari za kukata tamaa. Kwa hivyo Ayubu alimgeukia Bwana Mungu: “Hata sasa shahidi yangu yuko mbinguni, wakili wangu yuko juu. …. macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu (Ayubu 16: 19-20). Mfalme Daudi alikuwa amezungukwa na watu kila mara, alikuwa na familia kubwa na wafuasi wengi, lakini tunamsikia akilia kama Ayubu: “Nitaenda kwa nani?” Daudi awasihi watu wa Mungu kufanya vile Ayubu alifanya “Enyi watu, mtumainini Yeye, wakati wote, mmiminieni Yeye mioyo yenu, kwa kuwa Mungu ni kimbilio letu (Zaburi 62:8).&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Wapendwa, mifano hii ni Mwito kutoka kwa Bwana. Anakusihi kutafuta mahala kimya pale unaweza kumlilia kutoka kwa nafsi yako. Ayubu na Daudi “walimwaga shida zao” walipokuwa taabani, nawe pia unaweza. Unaweza kuongea na Yesu kuhusu shida zako sasa hivi, mwambie vile imechoshwa na kufa moyo. Tangu enzi za jadi, Mungu amewajibu wote walio amini ahadi zake. Atasikia kilio chako pia, kwa Upendo na Huruma. Hata wahi kudharau kilio chako. Yeye atakupa nguvu mpya kwa kila tabu.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;5. Tujipeana kamili kwa Bwana katika kila jambo&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Yesu alitabiri kuja kwa shida duniani: “Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa …Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za vitu vya angani zitatikisika (Luka 21:25-26). Kristo alikuwa akieleza kwamba, “bila Matumaini ndani yangu, wengi watakufa kwa Uoga.” Bali kwa wale wanaomuamini, ameahidi kuwachunga, kuna Uhuru unaoshinda Uoga. Kwanini? Uhuru wa Ukweli huja pale tunapo jipeana kabisa mikononi mwa Bwana. Kujipeana kabisa ni tendo la Imani. Inamaanisha kujiweka chini ya nguvu zake, Hekima na Msamaha wake. Ina maanisha kuongozwa katika matakwa yake.Tukifanya hivi, Mungu ameahidi kuwa Mchungaji wetu – kutulisha, kutuvalisha na kutupea makao, na pia kuchunga Mioyo yetu kutokana na maovu.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Yesu ni mfano maalum wa kujipeana alipoenda msalabani. Kabla tu akate Roho, alilia, “Baba, mikononi mwako naikabidhi roho Yangu.” (Luka 23:46). Kristo aliweka maisha yake yote katika mkono wa Baba. Kupitia kitendo hicho, aliweka nafsi zote za wafuasi wake, kondoo wake wote katika mikono ya Baba. Tunapoambiwa tuweke maisha yetu katika mikono ya mtu mwengine, ni lazima tuhakikishe kuwa ana nguvu za kutuchunga kutoka kwa maadui, janga na vita. Paulo alitoa ushuhuda, “ninamjua Yeye niliyemwamini na kusadiki ya kuwa anaweza kukilinda kile nilichokiweka amana Kwake hadi siku ile. (Timotheo wa pili 1:12).&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;6. Tuishi kila siku katika kumuhofu na kumuheshimu Bwana.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Nabii wanaonya kwamba Mungu hutikisa mataifa, lazima tutavutwa kumuhofu.&lt;/p&gt;
&lt;ul&gt;
&lt;li&gt;Ezekieli aliuliza, “Je, ujasiri wako utadumu au mikono yako itakuwa na nguvu siku hiyo nitakapokushughulikia? (Ezekieli 22:14).&lt;/li&gt;
&lt;li&gt;Mungu alipo muonya Noah kujenga Safina kwa sababu ya hukumu “Noah alimcha Mungu” (Waibrania 11:7).&lt;/li&gt;
&lt;li&gt;Ata Daudu jasiri alikubali, “Mwili wangu unatetemeka kwa kukuogopa wewe (Zaburi 119:120).&lt;/li&gt;
&lt;li&gt;Habakuki alipo ona utabiri ya hukumu ya siku zijazo, alilia, “Nilisikia na moyo wangu ukagonga kwa nguvu, midomo yangu ikatetemeka kwa hofu niliposikia sauti, uchakavu ukanyemelea mifupa yangu, na miguu yangu ikatetemeka. Hata hivyo nitasubiri kwa uvumilivu siku ya maafa” (Habakkuki 3:16).&lt;/li&gt;
&lt;/ul&gt;
&lt;p&gt;Elewa kwamba, Uoga uliokuwa na hawa watu wa Mungu sio Uoga wa kimwili, lakini ule Uoga wa Kumcha Mungu. Waumini hawakuogopa maadui wa Nafsi zao, waliogopa hukumu ya haki kutoka kwa Mungu. Walielewa vyaema Nguvu zilizo nyuma ya yale mateso yanayokuja. Hawakuogopa matokeo ya gharika, walihofu tu Utukufu wa Mungu. Kila mmoja wetu atapata Uoga siku zijazo. Lakini Uoga wetu uwe ule wa Kumcha Bwana, sio wa kimwili kuhusu kushuku ahadi za Bwana. Dunia nzima watu wamejaa Uoga wa kimwili, wanapo ona Uchumi ukidhoofika. Wanahofu kwamba gharika la uchumi litafagia yote yale wamekusanya. Hiyo ndio kilio ya wasio amini. Sisi tuko na Matumaini, kilio kama hicho hakifai kuwa na waumini.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Kama wewe ni mwana wa Mungu, Baba yako aliye Mbinguni hata stahimili shaka kama hiyo. Isaya anaonya: “Mimi, naam Mimi, ndimi niwafarijie ninyi. Ninyi ni nani hata kuwaogopa wanadamu wanaokufa, wana wa wanadamu ambao ni majani tu, kwamba mnamsahau BWANA Muumba wenu, aliyezitanda mbingu na kuiweka misingi ya dunia, kwamba mnaishi katika hofu siku zote kwa sababu ya ghadhabu ya mdhalimu, ambaye nia yake ni kuangamiza? Iko wapi basi ghadhabu ya mdhalimu? (Isaya 51:12–13). “BWANA Mwenye Nguvu ndiye peke yake ikupasaye kumheshimu kuwa mtakatifu, ndiye peke yake utakayemwogopa, ndiye peke yake utakayemhofu (8:13). Tunapasa Kumhofu na Kumcha Mungu pekee.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;7. Tuwe na Furaha ndani ya Bwana.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Amani tuliyo nayo inategemea kujipeana kwetu katika mikono ya Bwana, haijalishi shida tulizonazo. Zaburi inasema, “Jifurahishe katika BWANA naye atakupa haja za moyo wako. (Zaburi 37:4). Kama umejipeana Kamili kwa Bwana, atakutweka nguvu kuvuka shida zote. Lengo lake ni wewe uweze kufanya mambo yako ya kila siku bila Uoga au hofu, ukiamini tu Uchungaji wake. Kujipeana kwako kutakuwa na matokeo maalum katika maisha yako. Unapojipeana katika Uchungaji wa Mungu utaweza zaidi kuepuke misukosuko inayokuzunguka. Ukijipeana kwake, huta ogopeshwa na habari za kutisha. Hutakuwa ukijaribu kila wakati kutafakari njia ya kukwepa. Ni kwa sababu maisha yako, ya familia yako na maisha ya mbeleni yako mikononi mwa Bwana. Mchungaji wetu mkuu anajua kamili jinsi ya kuweka na kuhifadhi kondoo wake, kwa sababu anatuongoza kwa Upendo.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Nikimalizia, narudi kwa lile Swali la Yesu kwa Filipo: “Unafikiri tufanye nini?” Jameni jibu letu liwe hili: “Bwana, wewe ndiwe mtenda miujiza. Napeana shaka zangu zote na uoga wangu wote kwako. Ninapeana mikasa na maisha yangu katika uchungaji wako. Najua huta niacha nizimie. Kwa kweli, ninajua lile utakalo tenda kuhusu shida zangu. Ninaamini nguvu zako.” Amina!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;---&lt;br /&gt;Maandiko yamenakiliwa kutoka kwa IBS-STL Global translation http://www.ibs.org/bibles/swahili/index.php)&lt;/p&gt;</description>
 <category domain="http://www.worldchallenge.org/sw/taxonomy/term/275">David Wilkerson</category>
 <pubDate>Tue, 05 May 2009 19:33:19 -0500</pubDate>
 <dc:creator>thomas_rewe</dc:creator>
 <guid isPermaLink="false">6425 at http://www.worldchallenge.org</guid>
</item>
<item>
 <title>Habari ya Dharura</title>
 <link>http://www.worldchallenge.org/sw/node/6319</link>
 <description>&lt;p&gt;Nimeguswa na Roho Mtakatifu niwatumie ninyi nyote mulioko kwa mtandao wetu, kwa marafiki na maaskofu wale tumewahi kukutana kote Duniani.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;JANGA KUU LITAKALO TIKISA DUNIA NZIMA LIKO KARIBU KUTOKEA. LITAKUWA LA KUTISHA SANA, SOTE TUTATETEMEKA - ATA WALE WANAO MUHOFU MUNGU KATI YETU.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Kwa miaka kumi sasa nimekuwa nikiwaonya kuhusu Mioto elfu moja ya New York City, itakayo funika megacomplex yote, mpaka New Jersey na Connecticut. Migomo na Misukosuko ya watu itazuka katika miji mikuu hapa Amerika – kama yale ya Watts, Los Angeles miaka iliyopita.&lt;br /&gt;
Misukosuko ya watu na mioto itaikumba miji ya Ulimwengu. Kutakuwa na kuporwa kwa mali – hata hapa kwetu Times Square, New York. Yale tunayo yaona leo sio tu kudhoofika kwa Uchumi. Tuko katika Hukumu ya Mungu. Imenakiliwa katika Zaburi 11:3&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;“Wakati misingi inapoharibiwa, mwenye haki anaweza kufanya nini?’’&lt;br /&gt;
Mungu anahukumu dhambi za Waamerika na za Dunia yote. Anaivunja misingi ya Kidunia.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Nabii Yeremia aliwasihi waisraeli walipokuwa wamemuasi Mungu, ‘‘Basi kwa hiyo waambie watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu, ‘Hili ndilo asemalo BWANA: Tazama! ninaandaa maafa kwa ajili yenu nami ninabuni mabaya dhidi yenu. Kwa hiyo geukeni kutoka katika njia zenu mbaya, kila mmoja wenu, tengenezeni njia zenu na matendo yenu.’ Lakini wao watajibu, ‘Hakuna faida. Tutaendelea na mipango yetu wenyewe, kila mmoja wetu atafuata ukaidi wa moyo wake mbaya.’’ Yeremia 18:11-12)&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Katika Zaburi 11:6, Daudi anaonya, “Juu ya waovu atawanyeshea makaa ya moto mkali na kiberiti kinachowaka, upepo wenye joto kali ndio fungu lao.” Na ni Kwanini? Daudi ajibu, “Kwa kuwa BWANA ni mwenye haki, hupenda haki”. Hili ni tukio la Hukumu ya Haki Kutoka kwa Bwana Mungu kama alivyofanya Sodom katika kizazi cha Noah.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;WATAKATIFU WATAFANYA NINI? ITAKUWAJE KWA WATU WA MUNGU?&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Jambo la kwanza ni hili nililopokea kwa makusudi yangu mwenyewe, tenga kando kiwango cha siku 30 cha chakula isiyoweza kuharibika, vitu vya bafuni na choo na vitu muhimu. Katika Miji mikuu ulimwenguni, vitu hivi vitapotea madukani kwa upesi mno kunapotarajiwa Janga kuu.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Kiroho, tuko na njia mbili. Zimenakiliwa katika Zaburi 11:1 “Ruka kama ndege kwenye mlima” Au kama asemavyo Daudi, “BWANA yuko ndani ya hekalu lake takatifu, BWANA yuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni Huwaangalia wana wa watu, macho yake yanawajaribu. (mstari wa nne). “Kwa BWANA ninakimbilia” (mstari wa kwanza).&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Nita ambiya Nafsi yangu: Hamna haja ya kutoroka...hamna haja ya kujificha. Hili ni tukio la Haki kutoka kwa Mungu. Nitamtegemea Mungu aliye katika Kiti chake cha Enzi, macho yake ya Upendo na huruma yakitazama mienendo yangu – nikiamini ya kwamba atakomboa watu wake hata kutoka kwa Mafuriko, Mioto, Janga na Majaribu ya aina yote.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Zingatia: Sijui mambo haya yatatendeka lini, lakini najua hayako mbali sasa. Nimeeleza yote yale yaliokuwa mzigo katika Nafsi yangu. Fanya na habari hii vile utakavyo chagua wewe mwenyewe.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Mungu akubariki na akulinde.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Katika Kristo&lt;br /&gt;
DAVID WILKERSON&lt;/p&gt;</description>
 <category domain="http://www.worldchallenge.org/sw/taxonomy/term/275">David Wilkerson</category>
 <pubDate>Tue, 10 Mar 2009 11:43:27 -0500</pubDate>
 <dc:creator>thomas_rewe</dc:creator>
 <guid isPermaLink="false">6319 at http://www.worldchallenge.org</guid>
</item>
<item>
 <title>Watu Wa Mungu Hawata Aibika Katika Nyakati Za Janga Kuu</title>
 <link>http://www.worldchallenge.org/sw/node/6225</link>
 <description>&lt;p&gt;Nilipokuwa nikiliandaa neno hili, Gazeti la Wall Street Journal lilinakili kwamba Dunia nzima imefunikwa na wingu kuu la Uoga. Watu kutoka mataifa yote sasa wamebutwaa na matukio yalio ulimwenguni leo. Mara moja nilianza kuwaza kuhusu waumini wa hapa kwetu Times Square Church. Hawana uoga kama huwo. Ingawa tumemakinika na matokeo hayo, tuko pia na Furaha kuu. Nikaongozwa pale kwa Zaburi 37, ilioandikwa na Daudi: “BWANA anazifahamu siku za wanyofu, na urithi wao utadumu milele. Siku za maafa hawatanyauka, siku za njaa watafurahia kuwa na wingi wa vitu. Unabii wa ajabu kwa watu wa Mungu unaoendelea kutimizwa kati yetu hivi sasa. Kwa ufupi, Zaburi 37 inatueleza kwamba Mungu huinuka na kuhukumu Jamii ambazo dhambi zao zimeikera Mbingu. Daudi akatoa Unabii, “kwa maana nguvu za waovu zitavunjwa (Zaburi 37:17). Walakini, Zaburi hii iko pia na ahadi kuu kwa wenye haki walio mwamini Bwana. Kwanza kwaja nyakati ambapo Mungu hatastahimili tena uchoyo, tamaa na ufisadi ambazo waovu wametenda kwa maskini wasiojiweza. Unabii wa Daudi unanena kuhusu upotevu wa haraka wa nguvu za fedha. “Lakini waovu wataangamia: Adui za BWANA watatoweka kama uzuri wa mashamba, watatoweka, watatoweka kama moshi (Zaburi 37:20). Neno lanena kuhusu moto utakao choma mali na fedha zitakazo fifia kama moshi. Tafakari picha ya yale yalioitokea Uchumi wa Amerikani. Katika kipindi cha wiki mbili, zaidi ya takriban Trilioni 4 za dola za Amerikani zilififia. Sasa tunajulishwa kwamba trilioni zengine zitafifia pia kama moshi. Soko la hisa dunia nzima limeshikwa na butwaa na madalali wanalia wakipiga nduru. Sitaki kuifafanua sababu ya Mungu kuyakubali matukio haya, lakini nitasema hili: tunajua Mungu halali. Kunakuja kila mara kama vile asemavyo Isaya “Kwa sababu BWANA anayo siku ya kulipiza kisasi, mwaka wa malipo, siku ya kushindania shauri la Sayuni” (Isaya 34:8). “Mchana kutwa nimeinyoshea mikono yangu kwa watu wakaidi, wanaokwenda katika njia ambazo si nzuri, wafuatao mawazo yao wenyewe, taifa ambalo daima hunikasirisha machoni pangu, wakitoa dhabihu katika bustani na kufukiza uvumba juu ya madhabahu za matofali,… Tazama, jambo hili hubakia limeandikwa mbele zangu, sitanyamaza kimya bali nitalipiza kwa ukamilifu, nitalipiza mapajani mwao” (Isaya 65:2-3, 6)&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Tunayaona katika Uchumi wetu sio tu Kulipiza kisasi kwa Mungu, bali ni kuimarishwa kwa Heshima na Utukufu wa Mungu. Hatasimama tu pale njia zake zinapoporwa na waovu. Ezekieli akaandika, “Wakati umewadia, siku imefika. Mnunuzi na sifurahi wala mwuzaji asihuzunike, kwa maana ghadhabu iko juu ya kundi lote...Wajapo piga tarumbeta na kuweka kila kitu tayari, hakuna hata mmoja atakayekwenda vitani, kwa maana ghadhabu yangu iko juu ya kundi lote (Ezekilei 7:12, 14). Katikati ya uovu Mungu ameipiga tarumbeta ya onyo, lakini onyo halikupewa maanani. Paulo aandika kuhusu nyakati hizi akisema, “Lakini yakupasa ufahamu jambo hili, kwamba siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari... Lakini watu waovu na wadanganyaji watazidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika (Timotheo wa kwanza 3: 1, 13). Tafakari rahani za nyumba walizoshindwa kulipa, na malipo yalipokuja waliachwa bila manyumba. Benki za sifa zilianguka kwa sababu ya uongo, lakini wakuu wa hizo Benki walijipea pesa za “Parachuti za dhahabu” (golden parachute) ya mamilioni ya pesa. Nasoma kuhusu wakuu hawa wakiandaa maamkuli, wakidensi usiku mzima wakinywa pombe wakiwa na ufahamu kamili kwamba kampuni zao zilikuwa zimefilisika. Waliburudika vivlivyo ingawa walijuwa wengi watapoteza nyumba zao. Ni wazi kabisa kwamba unabii umetimizwa: Sefania 1:9 “hukwepa kukanyaga kizingiti (ya maskini), ambao hujaza hekalu la miungu yao kwa jeuri na udanganyifu. Tulifikiri Mungu atavumulia wazimu huu kwa mda gain? kuchafuliwa kwa jina lake? Mungu ndiye analo neon la uamuzi kwa jambo hili, na asema, “Katika siku hiyo nitaadhibu wote” (Sefania 1:9). Kwa ufupi: “Nitawaibisha!” “Lakini panga zao zitachoma mioyo yao wenyewe, na pinde zao (mali na fedha) zitavunjwa (Zaburi 37:15). Ata hivi ninaponena na kuandika neno hili, mabilionea wawili wamepewa dhamana kwa sababu mali yao yote imepotea kwa usiku mmoja.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Wakati ule Mungu analipiza kisasi kwa waovu, atatunuka wale wenye haki wanao muamini.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Jameni, hili ndilo kiini cha maubiri yangu: “BWANA humtegemeza mwenye haki…Siku za maafa hawatanyauka (Zaburi 37:17, 19). Utauliza, “la maanisha nini hili neno kwa kweli? Lina maanisha: Mungu ni muaminifu sio tu kwa kulipiza kisasi lankini pia kwa kuweka ahadi zake. Daudi anasema hivi, “tazama kila mahali vile Mungu alitenda Neno lake, maonyo yake sasa yametimia na kuelezwa kwa habari zenu, matendo yake katika vyombo vya habari, kwani Mungu hatalitimiza Neno lake kuwahifadhi wateule? Tafakari tena: haijalishi lile litakalo tokea ulimwenguni – haijalishi habari zikiwa za kutisha kiwango gani, haijalishi kiwango cha kutetemeshwa kwa ulimwengu, vile uchumi utaanguka – watu wa Mungu hawata aibika kamwe. Kwa kweli, Mungu atatenda kulingana na Imani yetu kulitimiza Neno Lake kwetu. Ndio tutasumbuka, lakini tutanusurika wale tunaomuamini Bwana. Dunia haitaweza kusema eti Mungu wenu hakulitimiza Neno lake. Usidanganyike, tutakumbana na mambo ya ajabu yasiowezekana hapa mbeleni. Lakini Mungu wetu asema yeye ni Mungu wa yale yasiowezekana, anatenda muijiza pale hamna jibu la kibanadamu. Na tena, yeye aweka Sifa na Uvumo wake kwa mikono ya waumini, akituita tumkumbushe ahadi zake. Ungefikiri, “lakini Mungu aweza kulitetea jina lake mwenyewe. Hanihitaji mimi” la sivyo! Mungu amechagua watu wake wawe ushuhuda kwa dunia iliyo kiziwi iliyokosa kugusika na Mungu. Na anatuita tumkabili waziwazi katika yale aliyoahidi. Ona basi, kwa macho ya ulimwengu, Mungu kila mara yuko majaribuni. Wanaangalia kila mara tunapokumbwa na mambo yasiowezekana, wanasema, “huyu mtu huimba kuhusu vile Mungu hutengeza njia ya kumkomboa. Sasa wacha tuone kama Mungu wake atamjibu. Atafaulu kushinda haya ama ataishia kwa aibu? Wale wasioamini nyakati za Yesu walisema haswa vivyo hivyo pale Yesu alikuwa msalabani. “Sasa tutaona. Itakuwa kufufuka ama aibu?” Yesu hakuwa kiziwi asiweze kusikia uchokozi huwo. Lakini alijua jambo wale wasioamini hawakulijua. Baba Yake hatamuacha katika aibu. Mungu hangesita kumkomboa kwa ajili ya Jina Lake.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Kuna nyakati zikaazo kana kwamba Mungu ametoweka. – wakati ambapo watu wake wanaachwa kwa aibu na kuvunjika moyo – lakini hadithi nzima haija malizika. (Msalabani ilikuwa nyakati kama hii). Jambo linalotuponyoka wakati wa shida ni kwamba Heshima ya Mungu ikotaabani. Na wakati wote katika Bibilia tunawaona watu ambao Imani yao duni ilikwamilia kumuamini Mungu katika nyakati za janga kuu. Hawa watumishi, bila haya, walimuita Mungu atende jambo, kwa kuweka Heshima ya Bwana katika Kigingi, lakini wakimuamini kabisa kwamba ataleta Ukombozi.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;1. Tafakari Mfano Wa Musa Pale Bahari Ya Shamu&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Hili lilikuwa haliwezekani kwa nguvu za binadamu, waisraeli walikuwa mbioni kutoroka majeshi ya Misri, walipokuwa wamefungiwa na bahari pande moja na milima pande nyingine, Musa alimkabili Mungu katika Ahadi zake. Alikuwa amekwisha tabiri kwamba Mungu atawaongoza waisraeli mpaka Inchi ya Ahadi. Sasa Heshima ya Bwana ilikuwa katika Kigingi waziwazi. Nasikia ripoti zikirudi kuwa Farao amewatega waisraeli. Wote huko Misri walitazamia kwamba Farao atawarudisha waisraeli wakiwa na mapingu. Sherehe zingepangwa kufurahia ushindi wa Farao, pakiwa na vinyago vya dhahabu vikiinuliwa juu ya Mungu wa waisraeli. Musa alifanyaje kulingana na haya? Akitazama bahari ile kubwa mbele yake, alilia, “Songa mbele!” Musa aliamini kwamba Mungu atawatunza, aliamini neno la Bwana kwamba atawaongoza waisraeli mpaka Inchi ya Ahadi, Alikiri “Najua Mungu ni Muaminifu, nitatenda kulingana na Neno lake.” Tafakari matukio ya Imani hii. Kama bahari ya shamu haingefunguka kimiujiza, Musa angedhaniwa kuwa mjinga. Waisraeli wangerudi kwa utumwa, na Mungu hangewahi tena kuaminika. Lakini sote tunajuwa lililotendeka siku hiyo. Musa alinyoosha mkono wake, maji yalipasuka na kutawanyika na watu wakatembea kwa ardhi iliyo kauka. Mimi ninawaambia, hakuna yule anaye muamini Mungu atakaye aibika. Atatimiza kwa ahadi zake kwa ajili ya Jina Lake.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;2. Tafakari Yoshua&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Siku sita waisraeli walizunguka kuta za Yeriko, wakisema, “kuta hizi zitaporomoka.” Kwa wale waliokuwa humo Yeriko ndani, mambo hayo yalikuwa ni ujinga mtupu. Lazima walikuwa wamecheka mno. Mwishowe, siku ya saba, watu wa Mungu waliamuriwa wazunguke, si mara moja, lakini mara saba. Wakati huu, labda ata waisraeli wenyewe walisikia kama wajinga. Labda walifikiri, “haliku tokea lolote siku sita. Sasa ni kama tunapiga ngumi ukuta. Tutaaibika kama kuta hizi hazitaanguka. Walakini fikira kama hizi hazikumsumbua akili Yoshua. Yeye alinena, “Najua lile nililosikia kutoka kwa Bwana Mungu, najua pia kuwa Anaweza”. Alimkabili Mungu kwa ahadi zake, akiweka utukufu wa Mungu taabani. Tunajua lililotokea. “Watu walipiga nduru makasisi walipopiga mbiu: kisha...kuta za Yeriko ziliporomoka chini ndiposa Waisraeli wakaliingia mji nakuliteka nyara” (Yeshua 6: 20). Watu wa Mungu wanapomkabili katika Neno lake, Hawezi kuwaaibisha.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;3. Tafakari watoto wakihibrania.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Danieli pamoja na wale Waibrania watatu walikataa kuabudu sanamu ya Nebukadneza futi 90 ya dhahabu. Walikaa ngumu hata walipohukumiwa kifo motoni. Mfalme muovu akinena, “Naye ni mungu yupi atakayeweza kuwaokoa ninyi, kutoka katika mkono wangu?” (Danieli 3:15), vijana hawa walimkabili Mungu kwa ahadi zake: “Ee Nebukadneza, hatuhitaji kujitetea wenyewe mbele zako kuhusu jambo hili, ikiwa tutatupwa ndani ya tanuru iwakayo moto, Mungu tunayemtumikia anaweza kutuokoa na moto, naye atatuokoa kutoka mkononi mwako, Ee mfalme. Lakini hata ikiwa hatatuokoa, Ee mfalme, tunataka ufahamu kwamba, hatutaitumikia miungu yako wala kuiabudu sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.’’ (Danieli 3: 16-18). Walikuwa na matumaini kuwa Mungu ataliheshimu Jina Lake, walikubali bila pingamizi kifo kwa moto. Viongozi Vigogo nchi nzima walikusanyika kuona Utengevu huu: Vibwana, Magavana, Mahakimu, Viongozi kutoka mikoa mbalimbali. Naye Nebukadneza akaamuru moto ishindikizwe mara saba kupita kawaida, ikawa moto zaidi mpaka ikawauwa hata wale waliokuwa wakiiasha. Mkusanyiko ulishtuka na kusema, “hawa vijana hawataishi, watakufa hata kabla ya kuingia pale motoni, hakuna mungu awezaye kuokoa kotoka kwa janga hili”. Kwa mara nyingine tena, Jina la Mungu lilikuwa taabani. Kama hangeingilia kati, jina lake lingedharauliwa dunia yote. Kwa kweli, Mungu hawaaibishi wale wanao muamini. Maandiko yanakili kwamba Yesu mwenyewe alitokezea motoni kuwalinda vijana wale na kuwafariji watumishi wake. Vijana wakihibrania walitoka motoni bila hata kunuka moshi.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;4. Tafakari Mfalme Hezekia.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Maandiko yasema Hezekia alimcha Mungu: Alishikamana na BWANA kwa bidii wala hakuacha kumfuata (Wafalme wapili 18:6). Alipokuwa akiongoza, Yerusalemu ilipata kuzingirwa na Waashuru, waliokuwa vigogo wa vita zama hizo. Jeshi hili kuu lilikuwa tayari limekwisha teka nyara Samaria na miji ya Yudea, na sasa ilibaki Yerusalemu waliokuwa wamekwishazingira. Kapteni wao akawika, “tumewashinda nguvu miungu ya nchi zote, sasa munafikiri vipi kwamba huyu Mungu wenu atawaokoa?” Kwa mara nyingine, Mungu mwenyewe alikuwa taabani, Uaminifu wake ulijaribiwa mbele ya Milki yote, mbele ya maadui wa Israeli, na hata watu wa Mungu, je ingelikuaje Asingelitenda kitu? Waovu wangecheka na neno la Mungu lingekuwa tupu bila maana. Janga lilipokuwa likiendelea kuwa baya, Nabii Isaya alitazama haya yote. Alikwsha pokea Neno kutoka kwa Bwana Mungu, akaliamini kabisa. Kisha akamkabili Mungu kwa Neno hilo, ili kumuhushumu Mungu. Akaomba, “Mungu heshima yangu haijalishi kitu. Usipookoa watu wako mimi naweza kujificha mwituni, ni Jina lako lililotaabani. Kisha akimueleza kwa upole mfalme Hezekia amjibu Kapteni wa Ashuru: ‘‘Hataingia katika mji huu wala kupiga mshale hapa. Hatakuja mbele yake akiwa na ngao, wala kuweka jeshi kuuzunguka. Kwa njia ile aliyojia, atarudi, hataingia katika mji huu, asema BWANA. Nitaulinda mji huu na kuuokoa, kwa ajili yangu na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.’’ (Wafalme wapili 19:32–34). Mungu hatakubali kamwe watu wake wanaomuamini waaibike, usiku huwo alitenda Miujiza ya ajabu. Maandiko yasema majeshi 185,000 ya Ashuru walikufa Kilingelinge, na kusababisha uoga mkubwa mpaka jeshi hili kuu la Ashuru likatimua mbio likihepa. Tena, Mungu alitetea watu wake kwa ajili ya Jina Lake.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;5. Tafakari Petro na Yohana katika agano Jipya.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Wafuasi hawa wawili walipokuwa wakielekea Hekaluni kuomba, walikutna na maskini mlemavu toka kuzaliwa kwake. Petro na Yohana labda walimpita mtu huyu mara nyingi mbeleni, wakati huu walisimama. Watu waliokuwa sokoni wakamsikia Petro akisema, ‘‘Tutazame sisi..... Kwa jina la Yesu wa Nazareti simama, uende.’’(Matendo ya Mitume 3:4, 6). Petro alimwita Yesu atende jambo, Utukufu wa Mungu menyewe ukiwa taabani. Labda watu walisema, “jameni muubiri mjinga namna ganai huyu, anamuamuru kilema toka kuzaliwa asimame na kutembea.” Natumai watu hawa walikuwa tayari kucheka na kuwadhihaki Petro na Yohana. Walakini miguu ya kilema huyu ilianza kusonga, kuanzia kifundo cha mguu ikielekea juu mpaka mapajani. Akachuchumaa, akajiinua juu nakusimama. Watu sasa walipigwa na butwaa, kilema huyu aliyeponywa akarukaruka kwa furaha. Ingelikuwaje kama Mungu hangetenda jambo? Hilo halikumsumbua Petro, alimkabili Mungu kutenda jambo. Mungu hawezi kuwaaibisha wale waliomuamini.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Sisi leo pia tunaweka Heshima na Utukufu wa Mungu taabani.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Tafakari matukio haya katika Bibilia. Katika kila hadithi, Sababu zote zilizo mfanya Kristo kuja na Kufa msalabani zilikuwa taabani. Walakini, katika Agano la Kale na Jipya, mipango na maono ya Mungu ilisimama na watu wa Mungu waliimarishwa. Katika hali zote, Mungu alitazamia watoto wake sio kumuamini tu bali kuamini pia uwezo wal´ke kutenda miujiza. Je, Mungu asitarajia haya kwetu? Tazamia Ushuda tuliompa Mungu, tumesema atakimu mahitaji yetu, tukamwita Yehova Jire. Tumenena ahadi zake za kukimu watoto wake. Sasa tena Heshima yake na Utukufu wake uko taabani. Tukimkabili atende, Mungu atuahidi: “Lakini kwa ajili ya jina langu nikafanya kile ambacho kitalifanya jina langu lisitiwe unajisi machoni mwa mataifa ambao mbele yao nilikuwa nimewatoa Waisraeli” (Ezekieli 20:14). Bwana asema, “Nilipowaokoa waisraeli sikuwa nimejificha mahali, nilitenda miujiza waziwazi diniani. Sasa nataka kutenda haya katika kizazi chenu”. Wapendwa, je unapitia janga ambalo hujamkabili Mungu? Je unaitwa uiweka imani yako kwa mambo usioweza kupanga? Umeafikia kwamba “ni Muujiza tu kutoka kwa Mungu itakayo niokowa sasa?” labda hatutaweza kujua vile Mungu atatenda miujiza yake; hamna yule alijua katika Biblia yote. Lakini twajua haya; malaika mmoja tu aweza kutorosha majeshi 185,000. Mungu hawezi kuaibisha watu wake!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Kwa sasa, anatuambia yale aliyowaambia Waisraeli, “Niliwaita kutoka kwa dhambi zenu. Nimewaimarisha wazi mbele ya wale walio karibu nanyi ili nilitukuze Jina Langu. Nimimi niliye kuita utoke nje, nanitakuokoa kutoka kwa waovu kwa ajili yangu mwenyewe.” Utatembea basi kwa yale unayo ubiri na kuyamini? Utamkabili Mungu kwa Neno Lake ili Jina Lake litukuzwe mbele ya Mataifa? Naomba tuchukuw Ombi la Daudi la Nyakati kama hizi: “Lakini Wewe, Ee BWANA, Mwenyezi, unitendee wema kwa ajili ya jina lako, uniokoe kwa wema wako: (Zaburi 109:21). Mungu hatawahi kuwaaibisha wale wanao muamini. Atalitimiza Neno lake kwa ajili ya Utukufu wake.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;---&lt;br /&gt;
Maandiko yamenakiliwa kutoka kwa IBS-STL Global translation http://www.ibs.org/bibles/swahili/index.php)&lt;/p&gt;</description>
 <category domain="http://www.worldchallenge.org/sw/taxonomy/term/275">David Wilkerson</category>
 <pubDate>Mon, 15 Dec 2008 13:50:25 -0600</pubDate>
 <dc:creator>thomas_rewe</dc:creator>
 <guid isPermaLink="false">6225 at http://www.worldchallenge.org</guid>
</item>
<item>
 <title>Wakati Wa Kilio na Wakati wa Vita</title>
 <link>http://www.worldchallenge.org/sw/node/5798</link>
 <description>&lt;p&gt;Nisomapo Agano la Kale, Imani yangu hupata nguvu na ule mfano wa Daudi. Jambo baya lilikuwa limemfanyikia mtu huyu, mpaka maisha yake yalikuwa yametishwa na wale waliokuwa wandani wake. Ninajengwa Imani na vile Daudi alivyo tafuta neno kutoka kwa Mungu wakati huu wa shida kuu. Ilikuwa hivi: Daudi pamoja na majeshi yake 600 walikuwa wanamtoroka Mfalme Sauli aliyakuwa akitaka kuwaua. Walifika mahali paitwapo Siklagi wakapiga kambi pamoja na familia zao. Kisha wakaenda vitani mabibi na watoto wakiwa wamebaki hapo kambini. Baada ya vita, Daudi na majeshi yake wakaanza safari ya siku tatu kurudi kambini. Kumbe wakati huo, kambi yao ilikuwa imetekwa nyara na kuporwa na Waamaleki. Adui huyu Mbaya aliteka nyara familia za Daudi na majeshi yake na kuchoma hema na kambi yote! Jaribu kutafakari tukio hilo pale Daudi na majeshi yake waliporudi: “Daudi na watu wake walipofika Siklagi, wakakuta mji umeangamizwa kwa moto na wake zao pamoja na wana wao na binti zaowamechukuliwa mateka” (Samueli wa Kwanza 30:3).&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Watu hao walipigwa na butwaa walipogundua hayo. Ilikuwa ni mgutuka wakutisha walishindwa kustahimili. Nawaona wakizungukazunguka bila mpango wakilia kwa uchungu. “lingefanyika vipi hili? kwanini Mungu aliwachilia lifanyike?”  “Hivyo Daudi na watu wake wakapiga yowe mpaka wakaishiwa na nguvu za kulia.” (Samueli wa Kwanza 30:4). Tukio hili kutoka kwa maisha ya Daudi linatuonesha kuwa kuna wakati wa kulia panapotokea jambo la huzuni. Maandiko yanawataja majeshi ya Daudi kama “Mashujaa”, ikimaanisha wanavita waliopata sugu wasioweza kulia. Lakini tukio hili liliwafanya Mashujaa kulia kwelikweli. Walakini, halikuwa tukio dogo. Si kwamba walipoteza nyumba tu au mimea shambani ililowafanya Mashujaa wa Daudi kulia; kama ingelikuwa hayo, wangepona kwa haraka. Lakini, ilikuwa ni hatari iliyokuwa inawakumba bibi na watoto wapendwa iliyowadunga Nafsi zao. Yaliyofuata yangeishia vibaya kwa Daudi: “Daudi alihuzunika sana kwa sababu watu walikuwa wakisemezana juu ya kumpiga kwa mawe, kila mmoja alikuwa na uchungu rohoni” (Samueli wa Kwanza 30:6).&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Tunayoyashuhudia duniani leo yamenakiliwa kwa maandiko: “Kwa sababu BWANA anayo siku ya  kulipiza kisasi,mwaka wa malipo, siku ya kushindania shauri la Sayuni.” (Isaya 34:8).&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Naamini kupitia misukosuko na balaa zilizoikumba ulimwengu, Mungu ana hukumu tamaa, wivu na majivuno. Ninahakika Hawezi tena kukubali uchafu wa ngono kuharibu Nafsi za kizazi chote. Na ninaamani kwamba ndoa ya ushoga imekuwa kiini cha hikumu hii ya Mungu. Nyakati anazonakili Isaya zilikuwa na kilio, majonzi na uwoga. Walakini, Mungu alimpa Isaya Neno la kujenga moyo akisema, “Itieni nguvu mikono iliyo dhaifu, yafanyeni imara magoti aliyolegea, waambieni wale wenye mioyo ya hofu, “iweni hodari, usiogope, tazama, Mungu wenu takuja, pamoja na malipo ya Mungu, atakuja na kuwaokoa ninyi.’’ Ndipo macho ya vipofu yatafumbuliwa na masikio ya viziwi yatazibuliwa.” (Isaya 35: 3 – 5). Mungu alikuwa anasema kwa hakika: “wainueni moyo waliochoka. Wajengeni wale waliodhoofika kati yenu. Watieni moyo walio na uoga and masononeko. Waambieni, hamna chanzo cha kuwa na uoga. Haya yote yameletwa na Mungu, na kupitia haya, atawakuza watu wake. Anafanya yote haya kuwaokoa ninyi. Wapendwa. Ata wale watakatifu mno kati yetu huingiwa na uoga moyoni pale mikosi inapokuja. Wakati kama huwo, Si dhambi kuwa na uoga kiasi. Kwa kweli, Mungu alipo mpa Isaya neno hili, alikuwa akihakikisha kuwa, wale mabo walikuwa wamepigwa butwa na uoga kwa sababu ya tendeko la ajabu wasiweze kumalizwa na tendeko hilo. Alitaka kila moyo uliokuwa na majonzi usikie: „Usiogope! Kuwa Jasiri, kwa kuwa Mungu ni Mwokozi kwa watu wake.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Baada Ya Wakati Wa Kilio, Huja Wakati Wa Vita&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Wakati hufika ambapo kilio chote mpaka kiishe. Wakati huo watu wa Mungu huinuka kutoka kilioni, kutoka kwa masononeko, kutoka kwa upungufu wa aina zote na kuchukua fursa vitani! Katika Agano Jipya, Waebrania anaitikia maneno ya Isaya: “Kwa hiyo itieni nguvu mikono yenu iliyo dhaifu na magoti yenu yaliyolegea. Sawazisheni mapito ya miguu yenu, ili kitu kilicho kiwete kisidhoofishwe bali kiponywe.” (Waebrania 12:12–13). Maanake, “usibaki chini, simama upiganiye Imani yako!” tumikia Imani yako ndani ya Bwana. Usikubali magoti yatikiswe, bali endelea kutimua mbio, ukitegwa na uoga na uanguka, Imani yako inaweza kupoeshwa”. Tafakari tabia ya Mashujaa wa Daudi baada ya tukio lile la kusikitisha. Baada ya kulia majeshi hawa walichukizwa na kuingiwa na hasira. Wakaanza kumlaumu Daudi, walikuwa wamepotoka, wenye chuki kutokana na shida ile, wakaanza kuokota mawe ili wamuuwe Daudi. Kwa maoni yangu, hili ndilo watendao wengi wakati huu wa Janga hili la Uchumi. Wamepofushwa na hasira yao, wanageuka kushoto na kulia wakiuliza, “nani chanzo la janga hili? Watupe wote jelani!”. Ninahimiza wafuasi wa Yesu: sahau vile tulifika hapa. Sahau kabisa kuhusu nani mwenye lawama. La muhimu zaidi, sahau kabisa kusema laiti ingelikuwa: “laiti ingelikuwa kwamba ningefanya hivi ama vile, pesa zangu zingelikuwa salama”. Ukikwamilia mawazo hayo, uoga wako utageuka na kuwa chuki na hasira au roho nyingine chafu ya kuzimu. Hapana! Mungu anataka kugeuza njia, Neno linatueleza, “sasa ndio wakati wakupigania Imani yako!”. Tazamia jawabu la Daudi: alijitia moyo. “Daudi alihuzunika sana kwa sababu watu walikuwa wakisemezana juu ya kumpiga kwa mawe, kila mmoja alikuwa na uchungu rohoni kwa sababu ya wanawe na binti zake. Lakini Daudi akajitia nguvu katika BWANA, Mungu wake. (Samueli wa Kwanza 30:6). Badala ya kuingi uoga, Daudi aliamua kupigana na uoga wake. Naamini alifanya hivi baada ya kukumbuka Uaminifu wa Mungu mara nyingi alipomkomboa kutoka kwa mambo ya kutisha katika maisha yake. Utotoni mwake, Daudi aliua kaka dubu, aliuwa simba na akammaliza jitu Goliathi. Sasa alitafakari vita hivi na nyingine alizoshinda. Kila Ushindi uliletwa tu na Imani yake isiyo tingisika. Daudi alisema: “Nahitaji Neno kutoka kwa Bwana Mungu”. Alijua hakuna mwengine anayeweza kumtia moyo – sio Kuhani wake, Abiatha hata Makapteni wa jeshi lake, hapakuwa na Mshauri kamwe. Ilimlazimu Daudi apate neno kwa yule mmoja aliyemkomboa kutoka kwa majanga yote aliyowahi kupitia. Wapendwa, hivyo ndivyo inafaa kwangu mimi na wewe pia. Hakuna mtu yeyete duniani awezaye kuinua roho yako unapokufa moyo. Hakuna awezaye kuikuza roho yako unapopitia janga. Inatulazima kila mtu tupate neno la kipekee kutoka kwa Mungu. Kama Daudi, tumeitwa tujutie moyo kwa kukumbuka yale makuu Mungu ametenda maishani mwetu. Na lazima tukumbuke nyakati zile Mungu amekuwa wa msaada toka enzi za jadi.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Kuinuana Moyo Kunaweza Tu Kutufikisha Umbali Kiasi.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Kama maubiri usikiayo kutoka kwa Mchungaji wako yana upako, basi yataweka maisha ndani yako. Mauburi katika Neno la Mungu hutia moyo watoto wa Mungu. Sawa tu na vile kuomba na kuabudu kwa pamoja huinua nyoyo zetu kwa mda. Walakini, haraka mno tunashushwa moyo wakati ibada ya juma pili inapokwisha. Jumatatu na jumanne hupita na habari katika runinga zinaaza kuchafuka na wengi tunarudi kwa uoga na kuangaika. Nyakati za kawaida, naweza kupokea ushauri kutoka kwa Mke wangu iliyeokoka, Gwen. Yeye huwa karibu kunipa Neno zuri wakati ninapolihitaji. Namuona vile daudi alivyomuona Abigaili, “Ndipo Daudi akapokea kutoka mkononi mwake kile alichokuwa amemletea naye akasema, “Nenda nyumbani kwako kwa amani, nimesikia maneno yako na kukujalia ombi lako.” (Samueli wa Kwanza 25:35). Lakini mambo yaweza kuwa magumu wakati wa janga. Wakati Imani yetu inapigwa vita – wakati maisha yetu yanapotishwa – mashauri ya mke au mume, wachungaji na marafiki wenye hekima yaweza tu kutufikisha umbali kiasi. Nyakati hizi ni nyakati za shida mno, ukweli ni kwamba, ni Neno la kibinafsi kako kutoka kwa Mungu ndilo liwezalo kutupitisha tukiwa na matumaini ya kudumu. Mungu amekuwa imara na muaminifu kwa kunena Neno kwa watu wake tokea enzi za jadi. Katika Agano la Kale, tunasoma mara nyingi: “Neno la Mungu Likaja...” Maandiko yanasema kuhusu Abrahamu: “Baada ya jambo hili, neno la BWANA likamjia Abramu..:” (Mwanzo 15:1). Tunasoma kumuhusu Yoshua: “Lakini Israeli wakajichukulia mifugo na nyara za mji huu, kama vile BWANA alivyokuwa amemwagiza Yoshua.” (Yoshua 8:27). Na vivyo hivyo ilikuwa na Daudi na manabii wa Mungu. Tunasoma maandakio, “Neno La Mungu Likamjia...” na kwa watu wa Mungu leo, tuko naye Roho Mtakatifu awezaye kunena neno kutoka Mbinguni kati yetu. Kupitia Roho Mtakatifu, faraja, uponyaji na Neno la kutuelekeza liko kwa wale wanaomuamini.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Tafakari wale majeshi 600 waliomfuata Daudi. Walisikia Maneno yale Mungu alimpa kiongozi wao. Lakini Maneno hayo yangetakiwa kwanza yawe hai ndani yao. Ilalazimu iwe kwamba Mungu aongee ndani ya roho zao kibinafsi. Ndio wangeliweza kupata nguvu za kupigana vita. Ndiposa naamini kwa wakati huu, changamoto kwa muamini yeyote yule, ni kukaa katika neno la bwana mpaka Roho Mtakatifu alifanye neno lichangamke na kutoka kwa karatasi za Bibilia mpaka kwa muumuni binafsi. Tutajua linapotendeka kwa sababu tutasikia sauti ya Roho Mtakaitfu iliyo tulivu ikinena ndani “Ahadi hii ni yako. Ni neno la Mungu kwako, lililoletwa likupitisha katika nyakati za shida.”&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Daudi Alijitia Moyo, Akarejesha Ujasiri Na Papo Hapo Akatenda Kulingana Na Imani Yake.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Daudi aliporejesha ujasiri wake, aliitisha Kisibau. Hii ilikuwa nguo maalum inayovaliwa kifuani mwa Kuhani iliyokuwa na mawe mawili. Wakati mwingi, Mungu alinena kupitia Kisibau. Na Daudi aliamua kupata Neno La Bwana la kumuelekeza mbele. “Kisha Daudi akamwambia kuhani Abiathari, mwana wa Ahimeleki, “Niletee kile kisibau”. Abiathari akamletea, naye Daudi alimwuliza BWANA, “Je, nifuatie kundi hili la wavamizi? Je, nitawapata?” (Samueli wa Kwanza 30:7–8). Tafakari mambo Daudi alifanya hapa, baada ya kulia, alirejesha nguvu, kisha akapiga magoti mara moja. Mungu akampa Neno la kumuelekeza, Mungu alimjibu ”Wafuatie. Hakika utawapata na utafanikiwa kuwaokoa” (Samueli wa Kwanza 30:8). Neno la Mungu kwa Daudi lilikuwa “enenda, utapata ushindi”. Kwa njia nyingine: “Kaa ngumu vitani, usife moyo!” Tunasoma yafuatayo katika Maandiko, “Daudi pamoja na watu wake 600 wakafika kwenye Bonde la Besori,” (30:9). Daudi mara moja alitenda kulingana na Neno la Mungu, lakini mimi nashangaa Daudi alijuwaje mahala pa kuenda? Ni njia gani angelifuata ili apate kurejesha yote yaliyoporwa? Ninaamini kulikua na Sauti nyuma ya Daudi ikimnenea, “hii ndio njia, pita hapa” wapendwa, vivyo hivyo ndivyo ilivyo kwetu wakati huu. Kanisa nyingi huimba nyimbo hii inayojenga moyo sana, “He will make a way,- Mungu atajenga njia” na kwa kweli Bwana wetu atenda vivyo hivyo haswa. Jameni, Mungu alikuwa na mpangilio maalum hata kabla ya janga kutokea. Na mpangilio huwo unaendelea vilevile alivyoipanga hata katika majanga haya tunayo kumbana nayo. Ninahakika Neno alilowaza Daudi kila mara lilikuwa, “Utafanikiwa Kuwaokoa wote!” Daudi alijuwa vizuri kabisa hata pata tena nyumba yake iliyokuwa pale Sikilagi. Majeshi wake nao pia hawange rejesha nyumba zao, shamba na mali. Hayo yalikuwa yamepotea yote. Hapana, “yote” watakayofanikiwa kuokoa ilikuwa ni usalama na uzima wa jamii zao. Unaona sasa ufananisho na nyakati zetu? Watu hawa hawakuwa warejeshewe maisha yao ya kale. Hawakuwa warudi kwa maisha ya utulivu, maisha hayo ya kitambo yalikuwa yamepitwa na wakati. Hayo sio yaliokuwa yakiwasumbuwa Daudi na majeshi yake 600, walikuwa wakijali tu jamii zao –lililomuhimu – tutakuwa na usalama. Labda iliwabidi kukaa kwa Hema na wake na watoto wao baada ya hayo yote. Lakini Mungu aliwahakikishia kwamba watakuwa salama.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Mungu Hakumueleza Daudi Vile Atamkomboa Akiwa Pamoja Na Jamii Yake.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Wapendwa, Mungu hata tueleza vile atawashugulikia wapendwa wetu, hata tuonesha vile atatuweka salama katika nyakati za janga. Njia zake ni zaa ajabu mno, huwezi ata kutafakari, hatutaweza kamwe kuyafafanuwa maisha yetu yote hapa duniani. Kwa Daudi, ukombozi ulitoka mahala ambapo hangeweza kudhania: kijana Mmisri aliyekuwa akielekea kufa. Mtumwa huyu kijana alikuwa karibu kufa Daudi alipompata jangani na kumpa maji na chakula. Daudi alipomuuliza, “wewe ni nani?” natumai Mungu alimnong’onezea Daudi, “Daudi, huyu ndiye ukombozi wako!” jameni, lakustaajabisha vipi, njia za kumiujiza za Mungu! kijana Mmisri aliyekuwa kifoni ndiye alikuwa awaelekeze Daudi na majeshi yake kambini mwa Adui. Kwa ufupi, Mungu alimtumia kijana asiyekuwa hata na Jina kuongoza watu wake kuokowa yote.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Nikifunga somo hili, nitawapeleka tena kwa Isaya 35.4: “waambieni wale wenye mioyo ya hofu, “iweni hodari, usiogope, tazama, Mungu wenu atakuja, pamoja na malipo ya Mungu, atakuja na kuwaokoa ninyi.’’ Wakati dunia inapokumbwa na malipizo – wakati mambo yote yanaenda mrama – Mungu yuko katika juhudi ya kutuokoa. Anatumia hata misukosuko ya janga za ulimwengu kuleta wokovu. Yeye ni Muaminifu na ni Mwokozi, atawakuza watu wake, kupitia majanga yote.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Maandiko yamenakiliwa kutoka kwa IBS-STL Global translation http://www.ibs.org/bibles/swahili/index.php)&lt;/p&gt;</description>
 <category domain="http://www.worldchallenge.org/sw/taxonomy/term/275">David Wilkerson</category>
 <pubDate>Mon, 24 Nov 2008 17:17:25 -0600</pubDate>
 <dc:creator>thomas_rewe</dc:creator>
 <guid isPermaLink="false">5798 at http://www.worldchallenge.org</guid>
</item>
<item>
 <title>Jeshi La Mungu Lililofichwa Nyakati Hizi Za Mwisho</title>
 <link>http://www.worldchallenge.org/sw/node/6353</link>
 <description>&lt;p&gt;Kuna jambo la ajabu duniani leo! Mungu yukazini anatenda jambo kwa Ukimya mafichoni – jambo lakimiujiza, binadamu hawawezi kulitafakari. Walakini, jambo hilo litatikisa dunia nzima nyakati hizi za Mwisho. Mungu anatayarisha Jeshi dogo la nguvu kati ya Wakristo! Jeshi hili ndilo litakuwa makini mno dunia nzima na Mungu atakuja kuwaongoza kutenda maajabu na kutingisa kuzimu. Mungu atamaliza nyakati akiwa na Jeshi Mabakio walio Makini na wasio na Uoga.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Maisha yangu yote nimesikia hadithi za baba zetu wa jadi waliochukia dhambi. Hawa wanaume na wanawake walitwaa masaa na hata masiku wakifunga na kuomba. Walijua vyema sauti ya Mungu. Waliomba bila kusita na walikuwa na nguvu na uwezo wa kutengana na Usherati katika siku zao. Hawa wajadi sasa hawako tena. Lakini Mungu yuko katika harakati za kuinuwa Jeshi lingine – walakini jeshi hili jipya halitakuwa la wazee wenye nyele nyeupe kutoka Zayuni. Litakuwa la waumini vijana na wazee – wakristo wa kawaida waliomkwamilia Mungu! Ni huduma mpya mno iko karibu kuja!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Kanisa la Madhehebu liko karibu kufifia. Halina uwezo wowote wa kuigeuza Dunia, Halina nguvu za Krito. Makuhani wengi wanaanguka kila wakati – kwa Usherati, tamaa, kiburi na ngono za aina yote. Wachungaji wa kiinjilisti wameleta maburudisho na maonyesho katika madhabahu. Mchungaji mmoja akaringa, “Ninataka kuwaletea watu wa michezo ya Broadway hapa Kanisani”. Mimi najua makanisa ya Kiinjilisti ambapo takriban asilimia 50 ya waumini wao wamekwisha vunja ndoa. Mahali kwingine, inafika hata asilimia 80 kulingana na Barua za waumini ninazopata. Washerati, wapenda ngono na wachawi – yote haya yameinyemelea kanisa la Yesu. Wengine wananilaumu kwamba niko mkali sana kwa wachungaji. La sivyo – kwa sababu niko na wachungaji wengi wale wanao lia kama mimi kuhusu kuanguka kwa huduma enzi hizi zetu. Kuna Mabakio ya Wachungaji nchini mwetu. Nashukuru kwa kila moja wao. Ni wazi kwamba wachungaji wengi wanaelekea katika njia hii ya ulegevu na ufisadi na hata sasa Dunia inaicheka Nyumba ya Mungu. Shetani anaringa kwamba ameshinda vita kwa sababu ya utoaji mimba kisheria, ushoga, ulevi, kuabudu shetani na uisilamu.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Walakini Bibilia inasema tusiogope! Mungu yuko na mpango, na Mpango wake umeanza kuenea. Mpango huu uko katika Neno. Kwa kweli, kila pepo kuzimu anajuwa Mpango huu!&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Mpango Huu Wa Mungu Unapatikana Katika Sura Nne Za Mwanzo Katika Samueli Wa Kwanza.&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Nabii Samueli ni mfano wa Mabakio wa Mungu. Mungu alimchagua katika nyakati mbaya zaidi akamficha na kumfunza mpaka ikatimia wakati wa kufichua Jambo jipya! Mungu akamwambia Samueli, “Tazama, nipo karibu kufanya kitu katika Israeli ambacho kitafanya masikio ya kila mmoja atakayesikia yawashe”(Samueli wa Kwanza 3:11). Hili Jambo jipya lilipangwa kuwashangaza na kuwashutua wale watakao lisikia. Jambo hili lilikuwa lipi? Lilikuwa Hukumu ya Mungu kwa dini duni iliyoanguka – na kutayarishwa, kuinuliwa na kupakwa mafuta kwa Mabakio watakatifu!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Sasa tazama yale Mungu alitenda wakati wa Samueli, yeye hutenda haya katika kila kizazi. Wakati kanisa la kidini linapoanguka, kulegea na kuwa baridi, Mungu analitosa nje na kuinua lengine. Kila kizazi kimekuwa na mabakio watakatifu, wale waombezi walio karibu na Moyo wa Mungu. Eli na watoto wawili, Hofni na Finehasi, walisimamia Kanisa lililopotoka kwa njia za Mungu. Bibilia inatuelza “Wana wa Eli walikuwa watu wabaya kabisa, hawakumheshimu BWANA (Samueli wa kwanza 2:12). Vijana hawa walimdharau Mungu. Walitenda Usherati katika milango ya Hekalu! Wanawake walipokuja kumtumikia Mungu, wana wa Eli waliwatega kando na kuwahadaa. Watu hawa hawakumuhofu Mungu – walikuwa wanatumikia kana kwamba ni kazi tu ya kawaida.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Lakusikitisha zaidi ya yote ni kwamba Baba yao aliangalia kando! Eli alikuwa karibu miaka 90, alikuwa amenona, yuko starehe na mgumu wa moyo. Alikuwa amezoea nyama nono aliyopata kutoka kwa waototo wake. Eli alijua nyama hii imelaaniwa – lakini hakutenda lolote kuzuia watoto wake kuiba. Alifunga macho asipate kuona Usherati wao. Hii ndiyo picha ya uovu ambayo imekumba kanisa la leo. Madhehebu yanajadili kuwapa mashoga madhabahu. – na kuleta laana katika nyumba ya Mungu. Eli na watoto wake wanasimamia, ukuhani uliokufa, wenye mitindo baridi wanaobembeleza dhambi. Wanatenda tu sasa matakwa ya huduma. Wakiwa na uungu uliyokosa nguvu. Ni kwa sababu wamekuwa starehe pale walipo! Wamepoteza Mguso wa Mungu na sasa hawasikii tena sauti yake. Kwa sababu wanafungia macho maovu. Mungu akasema, “Kwa kuwa nilimwambia (Eli) kwamba ningehukumu jamaa yake milele kwa sababu ya dhambi aliyoijua, wanawe kumkufuru Mungu, naye akashindwa kuwazuia.” (Samueli wa Kwanza 3:13). Kwa sababu Eli alikataa kuhukumu na kusahihisha maovu, Mungu alimng’oa kutoka kwa Mamlaka yake ya kiroho. Hili ndilo linalotendeka sasa katika kanisa ka Yesu kristo.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Wakati mchache uliopita niliongea na wachungaji wa Kipentekoste waliotembelea kanisa letu. Nilipowaeleza kuhusu ukosefu wa Kukemea dhambi, mkuu wa kundi hilo aliangusha tu kichwa chake. Mchungaji mmoja akatubu: “Ndugu Dave, ninaogope kwamba nikisema ukweli, nusu ya waumini watatoroka.” Kila mmoja ya watu hawa walikuwa wapole sana kwa waumini wao – wakiogopa kuwakwaza! Naweza kusema kwa hakika, sijaona hata wazee kumi wenye nyele nyeupe walio na motisha ya kulia kinyume na dhambi. Majeshi wengi wa Mungu ni kana kwamba wamekufa kiroho au wanaelekea kufa. – wamejipanga mbele ya Runinga, wamevuja nguvu zote kwa roho za dunia hii. Wamekuwa Eli – wakilala fofofo, wakinona na kufanikiwa, waoga wa kupinga dhambi!&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Mungu Alikuwa Amechoshwa Na Kizazi Cha Eli!&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Mungu alituma Nabii kumuonya Eli: “Wakati unakuja nitakapozipunguza nguvu zenu na nguvu ya nyumba ya baba yenu, ili pasiwepo mtu katika mbari yenu atakayeishi kuuona uzee (Samueli wa Kwanza 2:31). Mungu alikuwa akisema, “Ninajitenga na Nyumba hii — ninatoa uwepo wangu, nitakufanya bila nguvu na kuhukumu wachungaji wako. Nitapatiana ibada zenu duni kwa adui! “nanyi mtaona huzuni katika makao yangu. …” (mstari wa 32).&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Wakati huu, pesa za Muungano wa makanisa zinatumiwa kusaidia wapiganaji vita ulimwenginu mwote. Na tunashangazwa ni kwanini Kanisa la Amerika halina mamlaka ya Kiroho wala Uongozi! Madhehebu mengi yamekuwa kama makaburi na nyumba ya maiti. Hazina maisha, wala nguvu kwa sababu Mungu amewakwepa! Kanisa la Eli – Kanisa la Shilo – ni mfano kama huu. Mungu alilihukumu na kulikwepa kanisa hilo, yote yakifanyika kwa siku moja. “...Israeli wakapoteza askari 30,000 waendao kwa miguu. 11Sanduku la Mungu likatekwa, na hao wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, wakauawa. (Samueli wa Kwanza 4:10–11). Mungu alisema: “Imetosha!” na katika siku moja, Sanduku la Mungu lilitekwa nyara. Inalingana na kotoka kwa uwepo wa Bwana. Utukufu wa Bwana ulutoweka – Ikabodi akazaliwa – na Mungu akahukumu huduma duni kwa haraka! Eli alisikia habari kuhusu Sanduku kutekwa nyara, “...Mara alipotaja sanduku la Mungu, Eli alianguka kutoka kwenye kiti chake kwa nyuma kando ya lango. Shingo yake ikavunjika naye akafa, kwa kuwa alikuwa mzee tena mzito. (Samueli wa Kwanza 4:18).&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Hili ni picha nzuri ya yale yanayo tendeka kati ya madhehebu Amerika. Dini iko katika hukumu – wachungaji wanaanguka kulia na kushoto, viongozi wao wamekufa kiroho. Utukufu wa Mungu umetoweka – na kanisa limejipatiana kwa adui!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Ni kama siku za Yeremia. Watu wa enzi hizo walisema, “tuko sawa – hatuko hatarini. Hatutapoteza wokovu wetu”. Lakini Mungu alinena kupitia Yeremia: “ ‘Je, mtaiba na kuua, mtazini na kuapa kwa uongo na kufukiza uvumba kwa Baali na kufuata miungu mingine ambayo hamkuijua, 10kisha mje na kusimama mbele yangu katika nyumba hii, inayoitwa kwa Jina langu, mkisema, “Tuko salama.’’ Salama kwa kufanya mambo haya yote ya kuchukiza? Je, nyumba hii, iitwayo kwa Jina langu, imekuwa pango la wanyang&#039;anyi kwenu? Lakini nimekuwa nikiona yanayotendeka! Asema BWANA. “ ‘Nendeni sasa mahali pangu palipokuwa huko Shilo, mahali ambapo nilipafanya pa kwanza kuwa makao ya Jina langu, nanyi mwone lile nililopafanyia kwa ajili ya uovu wa watu wangu Israeli. (Yeremia 7:9–12).&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Katika kila kizazi Mungu huonya kanisa baridi zilizo chafu: “Rudini Shilo – rudini katika kanisa la Eli. Tazama yale niliyoyatenda kwa Hofni na Finehasi! Tafakari yaliyotendeka nilipotoa Uwepo wangu, Utukufu wangu utaondoka kila mara dhambi itakapoingia kwenye Kambi!”&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Bali wakati kanisa la Eli lilipokuwa katika hukumu, Mungu alikuwa akishughulika na kuinua Mabakio takatifu! Samueli anasimamia Mabakio takatifu – mwili wa waumini unainuka kutoka kwa vifusi la kanisa zee lililokufa. Nataka kuwaonesha yale mambo muhimu katika Ukufunzi wa Mabakio watakatifu wa siku hizi za Mwisho&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;1. Mabakio Huzaliwa Katika Maombi Na Maombezi!&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Hana alimzaa mwanawe kwa machozi na Maombi: “Kwa uchungu wa rohoni Hana alilia sana na akamwomba BWANA. (Samueli wa Kwanza 1:10). Jaribu kutafakari mahala pale: Hana yuko kwa hekalu kila siku, magotini, mbele ya madhabahu, amevunjika kwa sababu hana mtoto. Anapolia, mke mwenza Penina – alimchokoza. “...Kwa sababu BWANA alikuwa amemfunga tumbo, mke mwenzake alikuwa anamchokoza ili kumwudhi. Samueli wa Kwanza 1:6)&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Kuna mambo matatu muhimu ningependa kusema kuhusu tukio hili:&lt;br /&gt;
Kwanza, Mabakio takatifu inayosimamiwa na Samueli, huzaliwa kwa Majonzi na Maombi&lt;br /&gt;
La pili, wale waombao na kulilia Mungu watachokozwa na maadui.&lt;br /&gt;
Na la tatu, Mabakio takatifu wa Mungu kila mara hukosa kueleweka! Tafakari yalimtendea Hana alipokuwa katika maombi:&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;“Alipokuwa anaendelea kumwomba BWANA, Eli alichunguza kinywa chake. 13Hana alikuwa akiomba moyoni mwake midomo yake ikiwa inachezacheza lakini sauti haikusikika. Eli akafikiri alikuwa amelewa naye akamwambia, “Utaendelea kulewa mpaka lini? Achilia mbali mvinyo wako.” (Samueli wa Kwanza 1:12–14). Eli alikuwa mbali na Mungu – alikuwa amekufa kiroho – alifikiri Hana amelewa! Akamueleza, “Mama, utaendelea kwa mda gani kuja ukiwa hivi kanisani, tupa chupa ya ulevi!” Jambo hili linanishangaza mimi! Eli hakuweza kukosoa watoto wake kwa ulevi na usherati – lakini alimdhania Mwanamke wa Mungu kuwa mlevi! Hakuna tofauti na siku hizi zetu. Wakristo walio Makini wamejipatiana kwa maombi, wanatembea wakiwa kando pamoja na Yesu – lakini wachungaji ndiwo hugeuka na kuwa vizuizi, wakiwahadaa na kuwadhihaki!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Hana alipokuwa mbele ya Madhabahu, alijaa Uchungu, alililia mtoto. Lote aliloweza kufanya ni kusongeza mdomo tu kulingana na majonzi yaliyomo Rohoni. Aliomba, “...Ee BWANA Mwenye Nguvu, laiti ungeangalia huzuni kuu ya mtumishi wako na kunikumbuka mimi, wala usimsahau mtumishi wako nawe ukampa mwana, basi huyo mwana nitamtoa kwa BWANA kwa siku zote za maisha yake, wala wembe hautapita kichwani mwake. (Samueli wa Kwanza 1:11). Kama utampenda Mungu kwa Moyo, Nafsi, Akili na Nguvu zako zote, Basi kama Hana, utasikia uchungu wa Mungu na Kanisa lake. Mungu alimsikia Hana! Hii ndiyo maana ya jina Samueli: “Mungu alisikia Maombi yangu!” Siku hizi pia, Mungu anasikia maombi ya wale wanaolilia kuzaliwa kwa Kanisa takatifu, Jambo jipya la Roho Mtakatifu. Waumini hawa wanataka kuona Mungu akitenda jambo la ajabu – na Mungu atasikia kilio chao! Kutoka kwa tumbo la uzazi wa kiroho ya majeshi wasiojulikana la waombezi, mwili wa waumini unaendelea kuzaliwa – Kundi la Samueli, wale waliojipeana kabisa kwa Mungu!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Mambo mawili kuhusu Mabakio takatifu wa Mungu:&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;1. Wanaomba kama Hana: Mzigo wao ni wa kimo kirefu na mioyo yao imechokorwa kwa sababu ya dhambi ilioko kwa nyumba ya Mungu.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;2. Na kama Hana, wamejipena kwa maombi kila siku. Si kana kwamba wako juu mara chini, moto mara baridi. Hapana – wamejipeana kamili kwa Mungu. Wanamuendea na kumwaga yote yalio moyoni mwao: Enyi watu, mtumainini Yeye, wakati wote, mmiminieni Yeye mioyo yenu…” (Zaburi 62:8). “Vitu hivi ninavikumbuka ninapoimimina nafsi yangu: …” (Zaburi 42:4).&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Samueli akawa shujaa wa maombi – mpaka waisraeli hawakumuuliza mashauri bali walimuuliza awaombee! Maandiko yanasema, pale watu walipotaka Mfalme, “...Kisha Samweli akamwomba BWANA na siku ile ile BWANA akatuma ngurumo na mvua. Hivyo watu wote wakamwogopa sana BWANA na Samweli. Watu wote wakamwambia Samweli, “Mwombe BWANA Mungu wako, kwa ajili ya watumishi wako ili tusije tukafa,kwa kuwa tumeongeza uovu juu ya dhambi zetu nyingine kwa kuomba mfalme.”(Samueli wa Kwanza 12:18–19). Kila mara tunaona watu wakimsihi Samueli, “Tuombee.” Ni kwa sababu walikuwa wameamini maombi yake! Na katika nyakati hizi za mwisho, kutakuwa na Mabakio ya waombezi ambao watatafutwa na watu kwa sababu ya maombi, watu watakimbia wakilia, “Najua mtu awezaye kumgusa Mungu!” Kushauri pekee haita tekeleza matakwa ya watu. Itakuwa ni maombi ya watu wanao jua mawazo ya Kristo.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Mkristo mpendwa, Mungu anataka kukufanya mtu huyo! Anataka uweze kumgusa na kumsikia. Anataka kukupatia Huduma kutumikia wengine walio na mizigo na majaribu. Unapowaombea, neno lake litakuja!&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;2. Mabakio Takatifu Wamefunzwa Kujua Sauti Ya Mungu!&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Mungu alikuwa haneni na waisraeli kwa sababu ya dhambi ya wakuhani na waumini. Bibilia inasema: “Katika siku zile Neno la Mungu lilikuwa adimu, hapakuwepo na maono mengi” (Samueli wa Kwanza 3:1). Lakini, katikati ya ukame wa Neno, Mungu alimnenea Samueli: “...BWANA akamwita Samweli ...........Wakati huu Samweli alikuwa bado hajamjua BWANA. Neno la BWANA lilikuwa bado halijafunuliwa kwake. (Samueli wa Kwanza 3:8, 7). Samueli alikuwa miaka 12 wakati huwo, ingawa alikuwa mtoto mtiifu, hakuwa ameijua sauti ya Mungu. Basi Mungu alikuja kando ya Kitanda chake na kumwita. Samueli alifikiri ni Eli anayemuita. Hakujua alikuwa anafunzwa kutofautisha sauti – kusikia moja kwa moja kutoka kwa Mungu.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Tafakari haya. Mungu alikuwa hamuongeleshi Eli! Kwa kweli, hadi sasa, ni Nabii mmoja tu alikuwa akisikia kutoka kwa Mungu – yule ambaye hakutajwa jina aliyemuonya Eli kwamba Mungu anataka kumuhukumu. Hata Nabii huyu alikuwa mtu, ni sauti ya mtu pekee Eli angeweza kusikia –kwa sababu alikuwa kiziwi kwa sauti ya Mungu! Ndivyo ilivyo leo! Huduma ya eli, imekufa kiroho na kulala, imepoteza umakini na mamalaka, nguvu zote za Mungu zimetoweka. Kanisa linahitaji leo Waume na Wake wanaoweza kusimama na Mamlaka ya kiroho – kwa sababu Neno wanalohubiri limeinuliwa katika maisha yao matakatifu! Waubiri wengi leo hawawezi kusimama mbele ya waumini na kusema, “Ndivyo asemavyo Bwana!” – kwa sababu hawako karibu na sauti ya Bwana! Kusikia kutoka kwa Mungu inachukua zaidi ya nyakati za kimya pekee. Inachukua zaidi ya kusema tu, “Ongea Bwana, kwa sababu mtumishi wako anasikia!” Hapana, hakuna mipangilio maalum ya kumsikia Bwana – hakuna mikakati ya Kufuatilia, kabla hujamsikia Bwana, inalazimu kuwa yeye Bwana anaongea nawe!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Eli labda angelichukua miezi kadhaa pekee, akilia, “Bwana, Ongea nami!” lakini hakuwa na nafasi ya kumsikia Mungu – kwa sababu Mungu alikuwa haongei naye. Mungu alikuwa anataka kuongea na Samueli. Anaongea na wale ambao wametayarisha mioyo yao kusikia! Wauburi walio chafuka akili hawata wahi kumsikia Bwana. Waumini wale wanaovunja ndoa, washerati, wanaofanya sana michezo, kujiburudisha na kujifurahisha hawatamsikia Bwana, lile atakalo wanenea ni hili, Tubuni, Rudini! Lieni!”&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Samueli hakuwa msomi wa kidini Mungu alipomuongelesha. Lakini alikuwa na moyo mkunjufu, wa upendo uliokuwa wazi kwa Bwana. Unafikiri ni kitu gani Mungu alimfunza Samueli alipomuongelesha? “Sitakaa na dhambi katika nyumba yangu! Sitafunga macho kwa dhambi kati ya watumishi wangu.” Kwa ufupi, Mungu alimwambia Samueli, “Nitamuhukumu Eli – kwa sababu yeye na watoto wake ni waovu, naye Eli hakutenda jambo kuwazuia! Ingekuwa vyema wakivuliwa nguo za utumishi na kuambiwa, “hamuwezi kuenda hapo patakatifu! Samueli, sasa nataka kukuonesha chuki yangu kwa dhambi ndani ya nyumba yangu. Nataka nikuoneshe ni vipi utawahi kusikia sauti yangu na kutembea nami!” Samueli lazima alishutuliwa na mambo Mungu alitamka baadaye: “Naye BWANA akamwambia Samweli: “Tazama, nipo karibu kufanya kitu katika Israeli ambacho kitafanya masikio ya kila mmoja atakayesikia yawashe.” (Samueli wa Kwanza 3:11). Samueli aligundua kuwa Mungu atamkana Eli, mtu ambaye samueli alikuwa ametazamia. Moyo wa kijana huyu lazima uliguswa kwa majonzi pale Mungu alipomnenea, “Nitawaharibu watumishi waovu, nakuinua watu wanaonitafuta!”&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Mabakio takatifu nyakati hizi za mwisho wanajua kwamba Mungu anahukumu kanisa. Na wanaijua mpango wa Mungu. Wanajua kwamba Mungu atazivunja na kubomoa huduma mbovu za watu waovu! Si ajabu Bibilia inasema Samueli aliongea mambo ya Ukweli – alikuwa amesikia kutoka kwa Mungu! Alikuwa amechukua mda akiomba, akimtafuta Bwana, akajifungia naye – na Mungu akamuongelesha kila wakati. Kuna watu watakatifu wakati huu ambao wamefunzika kuijua sauti ya Mungu. Waombezi hawa wanamwaga mioyo yao kwake – naye Bwana anaimwaga Roho yake kwao!&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;3. Mabakio Takatifu Watafunzwa Ukombozi Wa Kweli – Kupitia Ujuzi Wa Njia Za Bwana!&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Nimeonya mara nyingi, Amerika inaelekea Janga na Kuporomoka! Waubiri wa chuki kama Louis Farrakhan wamejulikana sana sasa kati ya waamerika wausi kulingana hata na Jesse Jackson. (Farrakhan sasa anjulikana kushinda Martin Luther King!). Radio nyingi za waamerika wazungu hata hapa New York zinaubiri chuki kwa waafrika. Labda umesoma au kusikia maubiri yangu kuhusu vita vya kikabila. Kwa sasa inakaa kana kwamba hili haliwez kutokea. Lakini pale uchumi utakapo fifia, kaa chonjo! Kutakuwa na “majeshi ya kikabila” – wazungu wakipinga waafrika, wafrika wakipinga wayahudi, wakorea wakipinga waafrika. Tunapitia wakati wa hukumu hadi neno Ukombozi litapata maana tofauti kabisa! Wakati uliopita, wakristo wamechukulia Ukombozi kama uponyaji wa kimwili – macho yakirejeshwa, miguu ikiponywa. Hapa karibuni kutatokea hukumu kutoka mbinguni mpaka Ukombozi mkuu utakuwa kutokana na Uoga na Vitisho! Ukombozi wakati huwo utakuwa ni kuwa na neno kamili kutoka Mbinguni. “Yesu alisema mioyo ya watu itawapotoka kwa uoga wa yale mambo ya kutisha itakayoikumba ulimwengu. Na kweli, watu watashindana kujua mpango wa Mungu, watakimbilia njia zote wakitaka kumsikia yule aliye tulia, aliye na Amani, asiye kuwa wazima, na watalia, “Niambiye, je ni Mungu anahukumu? Yataisha lini haya yote?&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Na unafikiri nani atakuwa na jibu? Wewe – Mkristo wa kawaida ambaye amejificha ndani ya Bwana! Utakuwa mtulivu na mwenye amani wakati mambo yanaporomoka – kwa sababu Mungu yu nawe, unasikia kutoka mbinguni. Aliwaonya nyote kwamba haya yatatendeka – na aka ahidi kuwatetea! Niko na maono mawazoni mwangu ambayo naamini yametoka kwa Bwana Mungu. Ni ya magari mengi yakitoroka New York...ya kambi ya magari New Jersey na Pennsylvania...ya watu wakilala kwa magari yao kwa mawiki, kutoroka misukosuko hii. Haya yatatendeka kwa miji mingine pia. Itakuwa Janga kupita yale tumekwisha wahi kuona. Lakini Mungu atawaweka tayari Mabakio takatifu – watu walio makinika, wakweli, walioimara kabisa! Kama Samueli, maneno yao hayatapotea ardhini!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Samueli alikuwa na majibu kwa waisraeli; aliwakabidhi Ukombozi wa kweli. Zaidi ya watu 50,000 walikwisha kufa kwa sababu ya kuchungulia katika Sanduku la Bwana. Pale sanduku lilipoenda watu walikufa kama nzi – hakuna aliyejua la kufanya. Watu wakasema, “Hukumu hii lazima iwe kutoka kwa Mungu! Nani ataenda mbele zake kwa niaba yetu?” kwa hivyo wakamtumania Samueli naye, akawaambiya, “nataka mkusanyike Mizpah. Hapo nitawaonyesha njia ya kutokea” Samueli alikuwa na maneno ya sawa kulingana na Janga lililo kuwepo. “Naye Samweli akawaambia nyumba yote ya Israeli, “Ikiwa mtamrudia BWANA kwa mioyo yenu yote, basi iacheni miungu migeni na Maashtorethi na kujitoa wenyewe kwa BWANA na kumtumikia yeye peke yake, naye atawaokoa ninyi na mkono wa Wafilisti.’’ Hivyo Waisraeli wakaweka mbali Mabaali yao na Maashtorethi nao wakamtumikia BWANA peke yake.” (Samueli wa Kwanza 7:3–4).&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Jibu halitapatikana kwa kuombea kila mtu, hata wakiwa dhambini kiasi gani. Hapakuwepo na Ukombozi kwa yeyote aliyetaka. Hapana – Samueli alilia, “Elekeza moyo wako sawa, na hukumu dhambi yako! Tayarisha moyo wako kwa Bwana! Kwanza dhambi lazima ikanywe, ihukumiwe na iachwe. “Kisha Samweli akasema, “Wakusanyeni Israeli wote huko Mispa nami nitawaombea ninyi kwa BWANA.’’ (Samueli wa Kwanza 7: 5). Watu wakafunga na kunyenyekea mbele za Bwana: “Walipokwisha kukutanika huko Mispa, walichota maji na kuyamimina mbele za BWANA. Siku hiyo walifunga na wakaungama wakisema, “Tumetenda dhambi dhidi ya BWANA.’’ Naye Samweli alikuwa kiongozi wa Israeli huko Mispa. (Samueli wa Kwanza 7: 6). Aliwahukumu – Samueli alifichua dhambi yao kambini! Ufifio wa ukweli ulifuata Kemeo la Samueli.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Mungu anatueleza, Kambi ka Samueli litaleta Ukombozo wa ajabu kwa nguvu za maombezi: “…Kisha Samweli akamchukua mwana kondoo anyonyaye na kumtoa mzima kama sadaka ya kuteketezwa kwa BWANA. Akamlilia BWANA kwa niaba ya Israeli, naye BWANA akamjibu. Wakati Samweli alipokuwa anatoa hiyo dhabihu ya kuteketezwa, Wafilisti wakasogea karibu ili kupigana vita na Israeli. Lakini siku ile BWANA alinguruma kwa ngurumo kubwa dhidi ya Wafilisti na kuwafanya wafadhaike na kutetemeka kwamba walikimbizwa mbele ya Waisraeli.” (Samueli wa Kwanza 7:9–10). Hii ilikuwa ngurumo kutoka mbinguni, ikifwatwa na Ushindi mkuu – watu wa Mungu walipata Ushindi! Ilitendeka tu kwa sababu mtu mmoja alijua jibu. Samueli alijua la kufanya – kwa sababu alisikia kutoka kwa Mungu!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Naamini Mungu atatumia Mabakio takatifu wake kutingisa umati wa watu, kuamsha wachungaji na makanisa. Majeshi haya yatarudisha mioyo ya wengi kwa Mungu kwa kuwaleta katika Toba – kupitia nguvu maombi na Kukemea kwa dhambi. Jirani zako na wafanyikazi wenzako wote watataka majibu. Wanakujua tayari kwa sababu ya Amani na Utilivu wako – siku moja watakuja mbio kwako, wakilia, “Neno gani kutoka kwa Mungu? Mungu anasema nini? Nikinena kuhusu Mabakio walio mafundishoni, si maansihi jeshi la waubiri neno, wainjilisti, au wamishonari. Ninamaanisha Mkristo wa kawaida – wanao mpenda Yesu, ambao wao wenyewe watakuwa vielelezo vya kimiujiza ulimwenguni, waliojaa Amani na Utulivu. Mungu hataki wasomi waliofunzwa na njia za kidunia. Anataka Waume na Wake waliofunzwa katika maombi na Roho Mtakatifu! Anatafuta wale waumini walio jificha pamoja naye, wakitayarisha mioyo yao mbele zake, wakisomea kusikia sauti yake.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Je, mambo haya yanalingana nawe? Maisha yako hivi sasa ni Ushuhuda Duniani palipo na kutikiswa na kuogopa kwingi? Nakusihi – nenda kando pamoja na Mungu ili akuongeleshe, muulize akueleze dhambi iliyo katika maisha yako. Acha kabisa yote yale Roho Mtakatifu atakusihi moyoni. Jitoe kwake na uanze maombi. Kisha utakuwa tayari kama Jeshi, katika Jeshi lake kuu la siku hizi za mwisho. Hallelujah!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;---&lt;br /&gt;
Maandiko yamenakiliwa kutoka kwa IBS-STL Global translation - &lt;a href=&quot;http://www.ibs.org/bibles/swahili/index.php&quot;&gt;http://www.ibs.org/bibles/swahili/index.php&lt;/a&gt;)&lt;/p&gt;</description>
 <category domain="http://www.worldchallenge.org/sw/taxonomy/term/275">David Wilkerson</category>
 <pubDate>Tue, 10 Feb 2009 15:16:02 -0600</pubDate>
 <dc:creator>thomas_rewe</dc:creator>
 <guid isPermaLink="false">6353 at http://www.worldchallenge.org</guid>
</item>
<item>
 <title>Wako Wapi Wale Wengine Tisa?</title>
 <link>http://www.worldchallenge.org/sw/node/5777</link>
 <description>&lt;p&gt;Tafakari tukio hili kutoka Luka 17: Yesu alikuwa akielekea Yerusalemu wakati kusulubiwa kwake kulikuwa karibu. Alipokuwa akipita katikati ya Samaria na Galilea, alikaribia kijiji fulani ambapo kulikuwemo Wakoma kumi nje ya kijiji hiki waliokuwa wamepiga kambi kwa uchungu na pia aibu kuu. Kwa kweli, tisa kati ya hawa Wakoma kuni walikuwa wayahudi na mmoja aklikua Msamaria. Kumbuka kwamba, Wayahudi wa siku hizo walikuwa hawawezi hata kuwagusa Wasamaria wacha hata kuishi nao. Yaonekana shida ya ukoma iliyowakumba watu hawa iliwalazimu kubeba pamoja shida hii ya Ukoma.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Kwa wale ambao wamesomea ugonjwa huu, angalau unaweza kutafakari hali duni ya watu hawa. Yale tuyaonayo kila siku hapa New York City tayari ni mbaya mno. Hapa “41st Street”, karibu na Lincoln Tunnel, majengo duni ya makaratasi yamepangwa njiani, utaona hapo godoro chafu zilizooza, matambara na takataka zimerundikwa juu ya majengo haya. Ni kama mji mdogo ulio jaa chawa, panya, madawa ya kulevya, pombe, Ukimwi na magonjwa mengine pamoja na vita bila mkomo. Walakini, niamini nikikueleza kwamba majengo haya duni ya New York ni Ikulu tukilinganisha na pale Wakoma wale walikuwa wamepiga kambi nyakati zile Yesu alipokutana nao. Watu hawa hawakuwa na usaidizi wa vilema kutoka kwa serikali yeyote, hawakuwa na mpango wa kula bure, hospitali wala malipo ya maskini. Walikuwa wametengwa kabisa kutoka kwa jamii. Walikuwa maskini waliotupwa nje – waliolazimishwa kuishi nje ya kijiji. Wakoma walitakiwa kisheria kukaa futi 200-300 mbali na watu wengine. Watu wanapopita karibu nao, ilitakikana wapige mbiu wakisema, “Wachafu, Wachafu!” Kutokana na mda wa Ukoma wao, wengi wa watu hawa walikuwa wamepoteza vidole vya mkono au mguu, masikio, meno, mikono na pua. Ngozi zao zilikuwa zimeoza – na mnuko mahala hapo ulikuwa wakushtua mno. Watu hawa waliombaa, kubambanya na kula chakula ambayo watu wengine wangekosa hata kuiangalia. Inawezekana watu hawa waliishi mapipani. Na tena jambo lakuwasikitisha mno ni kukumbuka wapendwa walioacha nyumbani walipohukumiwa na Kasisi kwamba wao ni Wakoma. Walipoteza mabibi wapendwa, watoto wenye furaha, makao, kazi na utumishi wa aina yeyote ile. Inawezana kwamba wengine walikuwa labda Wayahudi waaminifu waliofuata maagizo ya dini kikamilifu. Lakini sasa walikuwa wamepiga kambi nje ya kijiji wakiishi maisha ya upweke yenye aibu na majonzi chungu nzima.&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Ukoma Katika Biblia Imelinganishwa Wakati Mwingi Na Mfano Ya Dhambi&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Maandiko yatuonesha kwamba Mkoma ni mfano wa mtenda dhambi anaishi kwa aibu – aliyeporwa na kumalizwa na majiraha ya dhambi. Katika Ibada zetu hapa Times Sqaure Church mara nyingi mistari mitatu ya viti hapa mbele hukaliwa na watu waliokuwa “Wakoma” hapo zamani. Vijana wadogo kutoka Timothy House, walikuwa watumiaji wa madawa ya kulevya na walevi wa kupindukia. Ukoma wa dhambi uliwadai wengi wao yote waliokuwa nayo. Bibi, watototo, kazi, heshima, afya, akili timamu na usafi. Wengi waliishia wakiwa bila makao, wasiojiweza na wapotevu. Sijui vile hawa Wakoma wakumi walisikia kuhusu Yesu. Labda Mkoma mmoja shujaa wa Kutangatanga alipitia hapo na kuwaeleza kuhusu yale makuu Yesu alikuwa amewatendea Wakoma kutoka miji mingine. Hata hivyo, walipata kujua kuhusu Yesu, na kwamba Yesu atapitia hapo karibu na wao na walikuwa wakimgojea kwa hamu mno. Jaribu kutafari haya. Wamekaa pale, karibu na barabra kama iwezekanavyo, lakini futi 200 hadi 300 mbali na barabara inayo pitia watu. Wamepiga kambi usiku mzima. Jameni jambo la kusikitisha kweli kuwaona watu hawa! Wakoma kumi wanukao wenye ngozi iliyooza, wakielekea kufa, wameshikana wakiinuana wakingojea tu pale Yesu atapitia barabarani. Mara nyingi nimewaza moyoni, Wakoma hawa walimuona Yesu na wanafunzi wake wakija pale barabarani, wakaanza kupeperusha mikono yao iliyopooza. Je, inaweza kuwa walikuwa wakioneshana pande za mwili zilizokatika? Au walikuwa wakipeperusha matambara chafu zilizo raruka? Sijui walimwita vipi Bwana Yesu. Lakini Yesu alipokuwa karibu vilivyo, walipaza sauti wakilia, “Yesu, Bwana, tuhurumie!’’. Walikuwa hawa ombi pesa, au Ahera wakifa. Walikuwa wanalilia Huruma. Ni kana kwamba walikuwa wakiomba – “Yesu – itawezekanaje ukumbane na jambo la kusikitisha kama hili bila kuwa na Huruma? Utawezaje kutunyima jibu? Niko na hakika, Yesu hakusita wale kuangalia kando hata kidogo. Aliwaangalia nyusoni mwao na kwa Huruma na Upendo mwingi akasema, &quot;Nendeni mkajionyeshe kwa makuhani&quot; (Luka17:14).&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Unaweza kufikiria Wakoma hawa waliwaza nini? Turudi kwa Makuhani? Kwanini? Wao ndiwo waliotutazama na kunena kwamba sisi tuwachafu! Walitufurusha nje ya Mji. Sisi wote kumi tukijipeleka mbele ya mlango wake, atatutazama mara moja tu na kukashifu ufedhuli wetu. Hakuna yule ashawahi kupona Ukoma. Atafikiri tumekuwa wazimu. Lakini naamini kwamba Wakoma wote kumi walihisi mtiririko wa Maisha, Afya na Nguvu! Mmoja kausongesha mkono ambao hakuweza kitambo kuusongesha, mwengine akisikia Maisha yakibubujika moyoni mwake – na akaanza kurukaruka juu chini! Mmoja baada mwengine, wakaangalia mikono yao, nyuso zao – na ngozi zilizo parara na kuoza ikaanza kugeuka. Ngozi yenye afya ikaanza kufunika viungo vyao, nyuso zao – walikuwa wanapona!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Je unakumbuka wakati Yesu alipokuhurumia wewe? Vile ulihisi usafi na maisha mapya! Ulipiga mbiu kwa sababu ulihisi Nguvu za Yesu zinazo safisha? Ulihisi maisha mapya ndani yako? Watu hawa walilazimika kuhisi maisha hayo mapya! Uwe na hakika kwamba msisimko maradufu wa furaha ulisambazwa kati ya watu hawa, na wakalipuka na kelele za furaha! Ngozi iliyopara na kuoza ilikuwa inapona. Na pale kulikuwa na vidonda, kulifunikwa na ngozi mpya yenya afya mno!&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Yesu Aliwaambia Hawa Wakoma Kumi Jambo Lile Lile Awaambialo Wakoma Anapowaponya: “Nenda Ukajioneshe Kwa Kuhani Kama Ushahidi!”&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Katika Luka 5:14, Yesu alimueleza mkoma mwengine, “nenda ukajioneshe kwa Kuhani, na utoe sadaka ya Utakaso kama vile Musa alivyo waamuru, iwe kama Ushahidi kwao” (Luka 5:14). Hakuna Mkoma angewekza mara moja kurudi nyumbani kwake, Kanisani au kwa majukumu na haki za Agano. Ilimlazimu kwanza afanya mambo fulani. Kwanza, ni lazima atajwe kuwa Msafi na Kuhani – na jambo hili lilihitaji mipangilio ya sherehe za kidini za karibu siku nane. Ililazimika anyolewe kipara kabisa, aoshwe na kuchunguzwa kikamilifu. Kisha ifwatwe na utoaji wa sadaka, kunyunyiziwa kwa damu na mafuta, kupakwa mafuta, utoaji wa dhabihu. Baada ya haya yote, ilimlazimu kungoja tena siku nane kabla hajajumuishwa kwa Familia yake na kurudia mipangilio na haki za kidini. Kwa ujumla, siku kumi na sita zilihitajika kwa mipangilio na sherehe hizi za utakaso za ajabu mno! Sherehe hizi za kidini ni ishara – ishara ambazo hutumiwa kueleza watu kuhusu Utukufu wa Mwokozi Yesu. Yote haya yamenakiliwa kwa Walawi 14: na haya ndio Wakoma wale kumi walirudi kutimiza mjini.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Katika muda huwo, labda Yesu na wanafunzi wake walikuwa wameshakula chakula cha mchana, na walikuwa wameanza safari tena wakiwa mbali na kijiji hiki. Muda si muda wakasikia kelele nyuma yao, walipogeuka na kuangalia nyuma, walimuona mtu akitimuwa mbio akija kwao – akipiga nduru na kupeperusha mikono yake! Mmoja wa hao wanafunzi akasema, “ni mmoja wa wale Wakoma kumi kutoka kwa kile kijiji”. Na alipokuwa akikaribia, wakamsikia akipaza sauti, Utukufu – Utukufu kwa Yesu! Usifiwe Bwana! Ilikuwa ni yule Msamaria mmoja! Alipomfikia Yesu, alijiangusha miguuni mwa Yesu akalala kifudifudi na kulipuka tena kwa sifa na shukurani. Kutoka ndani ya moyo wake akamsujudu Yesu mwana wa Mungu aliye Hai. “wewe ni Mungu, hungeweza kufanya hivi kama hungekuwa mwana wa Mungu. Sifu Mungu, Utukufu kwa Mungu!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Yesu alimtazama nakumwambia, “Je,hawakuponywa wote kumi? Wako wapi wale wengine tisa? (Luke 17:17). Alikuwa anauliza, “kwanini wewe tu? Wako wapi wale rafiki zako niliyoponya?” wapendwa, hilo ndilo swali Yesu auliza hata leo! Kati ya wale maelfu na maelfu aliyowaponya na kuwaweka huru, ni Masalia tu wanaovutiwa kwake! Wako wapi wale wengine basi? Nitakueleza walipo – wako pahali sawa na wale Wakoma walioponywa: wamepotea ndani ya kanisa – wamemezwa na dini!. Ninaamini takwimu za Bibilia, na kama takwimu za hadithi hii ni sahihi, basi asilimia 90 ya wale wanaoguswa na Yesu hurudi kwa kanisa lilolokufa na kukauka mno! Hawamfikii Yesu – kwa sababu wamepotea katika dini! Wakoma hawa tisa walikuwa na haraka ya kurudi kwa maisha yao waliyokuwa wameacha mbeleni. Walisema, “lazima nirudi kwa mke wangu na jamii yangu. Nataka heshima yangu irudi. Nataka kurudi Sinagogu niendelee kusoma kuhusu kuja kwa Mwokozi wetu!”. Labda utasema, ni nini kibaya hapo? Si mtu ameamuriwa kuilisha jamii yake? Na Daudi pia aongea kuhusu kuwaza kwa undani mambo ya Mungu? Wakristo si pia wanastahili kuwa na motisha ya kufanya kazi kwa bidii? – kufanya vile hawa Wakoma walifanya? Kwani Yesu hakuwaambia waende kwa Kuhani? Ndio, yote hayo ni kweli – lakini yote huwa bure kabisa kama kwanza hatuta chukuwa fursa kumjua Yesu kibinafsi!&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Wale Wakoma Tisa Walikuwa Kweli Wameguswa Na Yesu – Walifanyika Kuwa Mashahidi Wa Nguvu Zake&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;“Enendeni...kwa Kuhani....iwe kama ushahidi kwao” (Luka 5:14). Kwa miaka mingi ijayo, Wakoma hawa watamiliki Ushahidi wa ajabu kweli. Wangeweza kwa maisha yao yote kueleza tu vile Yesu alitenda. “Nilikuwa wakati mmoja Mkoma, mwenye upweke bila matumaini – mchafu, mpotevu, nikielekea kufa. Lakini Yesu alikuja na kunitakasa. Nimeponywa sasa ya timia miaka ishirini na tano – sifu Jina la Bwana.” Yote hayo yaonekana bora, laniki shida ni kuongea kumuhusu mtu wasiyemjua kamwe – wakitoa Ushuhuda wa Nguvu za Mwokozi ambaye hawaelewi kitu kumuhusu. Wanamtaja akiwa mbali. Wangekueleza umbo Lake, vile anaongea, vile atembeavyo – lakini hawakusonga karibu Naye wala karibu na moyo Wake!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Jambo linalonisikitisha sana katika miaka yote yangu ya huduma ni kushuhudia kuchoka kwa wale waliokuwa watumizi wa dawa za kulevya na walevi waliyo kombolewa kimuijiza kutoka kwa maisha ya dhmabi mbaya na uhalifu. Wengi wao waliitwa na Mungu kuuburi Injili, lakini Makanisa na Wachungaji Merikani kwote hawakukoma kuwaita watoe ushuda wao. Walibembelezwa kutoa siri za maisha yao ya kitambo. Na baada ya miaka kadhaa, wengi wa watu hawa washuhudia jambo moja tu. “miaka kumi na tano iliyopita nilikuwa Kuwadi wa malaya. Nimeishi na makahaba na nimefungwa jela mara ishirini. Siku moja mtu akanieleza kuhusu Yesu – na nikatakaswa na kufanywa Upya.” Wapendwa, mamia ya watu hawa sasa wame choka na kuanguka kutoka kwa wokovu kana kwamba meli zao zimegonga mwamba. Hawana hata utu wa Kristo, hawana uhusiano na Mungu, kwa sababu wanaishi kwa ushuhuda mmoja tu wa kitambo mno. Hawakurudi kwa Yesu, hawakuweza kumjua.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Watu wengi uniuliza, kwa nini wale wanao okoka katika kazi zetu za Uinjilisti wasitoa ushuhuda wao kila wiki hapa Times Sqaure Church? Kwa kweli hawa wanaume na wanawake wanaushuhuda wa ajabu kweli ambazo hujawahi kusikia. Lakini sisi tunawatazamia mema na zaidi kuliko tu ushuhuda mmoja mzee uliyoisha ladha. Tunataka waendelee mbele na Yesu – waweze kusimama na kueleza mapya kuhusu matembezi yao ya kila siku na Yesu, kuhusu yale mambo Yesu amewafanyia leo! Tunataka wampate Yesu Kristo kwa wingi kabisa!&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Inasikitsha Sana Kuona Wokovu Wengi – Waliokombolewa – Wakitulia Na Kupotea Katika Msisimko Wa Ukristo Wa Kisasa!&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Watu wengine ni kukataa wamekataa kutembea na Yesu. Wanapendelea dini aliyokufa! Wanafurahia msisimka na utamaduni wa ibada za kidini. Jameni ukifikiri tu vile Wakoma wale tisa walihisi walipokuwa katika mikakati ya utakaso! Ilikuwa ni sherehe za ajabu mno! Kwanza, Kuhani alichukua ndege wawili, akaua mmoja juu ya kibakuli cha maji “ya uzima” na kuwachilia damu ya ndege huyo kutiririka ndani ya maji. Kisha akafunga Hisopo kwa mbao ya mti wa Mwerezi (karibu inchi kumi na sita) na kuifunga kwa yule ndege aliye hai akitumia pamba nyukundu. Mabawa na mkia wa Ndege huyu zilitumbikizwa ndani ya damu iliyochanganyika na Maji. Damu hiyo pia ilinyunyiziwa Mkoma aliyepona kwa kipaji chake na kwa viwiko vyake mara saba. Kisha ndege huyo aliyehai aliachiliwa kupeperuka wazi uwanjani. Baadaye, Mkoma huyo aliyepona aliosha nguo zake na kunyoa nywele zake ata pia kuoga kwa utaratibu na kisha alirudi mjini kwa kitengo cha siku saba. Siku ya nane, alirudi kwa Kuhani na wana kondoo wawili wakiume na kondoo mmoja wa kike asiyekuwa na mawaa. Alileta pia galoni 2.8 za unga na painti moja ya mafuta kama sadaka ya kuvunja sheria, sadaka ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa. Kuhani alichukua mafuta yale na kuyapaka kwa viganja vyake, na kunyunyiza mara saba chini kwa ardhi. Kisha alichukua damu ya mwana kondoo, alimgusa nayo Mkoma aliyepona kwa ndewe la sikio lake la kulia, gumba lake la kulia la mkono na mguu pia. Kisha kuhani alichukua mafuta na kumpaka tena sehemu hizi tatu, mafuta iliyobaki alimmwagia kichwani mwake.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Ilikuwa sherehe za ajabu kweli – Wakoma wale waliopona walijihisi wanadini vilivyo. Sherehe hizi za kidini zilisimamia mambo ya undani sana kiroho – Upako, Utakaso na damu ya mwana kondoo. Walakini, yote hayo yalikuwa ni mfano wa mauti!, Wakoma walitoka kuguswa na Yesu na kuelekea dini ya mauti iliyojaa mila na desturi. Kwa kweli walikuwa wamerudishiwa heshima zao, walikuwa wamerudi kwa maisha yao kanisani, walipata tena baraka za mali, lakini hawakupata kumjua Yesu! Je utauliza, kwanini Yesu aliwarudisha wafanya mambo haya ya kidini? Mimi ninaamini Kristo aliwatuma kwa Kuhani akiwa na matumaini kwamba Wakoma wale watakuwa na kiu ya kutambua maana ya Undani ya desturi hizi za kidini. “Maji yanayotiririka” – si Yesu alisema kuwa yeye mwenyewe ndiye Maji ya Uzima? Unyunyizaji wa damu – si Yesu alisema Damu yake itamwagwa, kwamba yeye Atasulubiwa? Mwana kondoo kuchinjwa – hiyo inamaanisha nini? Tazameni, hakuna Kuhani Israeli yote angeweza kuwaeleza Wakoma hawa maana ya desturi hizo za kidini. Walifanya tu kama mazoea. Yesu alitazamia kwamba Wakoma hawa watamrudia awafunze mwenyewe. Walipomlilia hapo kandokando ya Barabara, “Bwana tuhurumie!” walitumia neno lililosawa na kusema “Jemedari, Mwalimu!” walijua alikuwa na Ukweli wote – lakini hawakua na kiu ya Ukweli huwo.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Hawa Wakoma kumi wanawakilisha maelfu ya watu leo wanao kaa Kanisani wanaosikiliza wachungaji ambao wanaubiri mambo wasiyoyaelewa. Maubiri yaliyokauka, yanayopekecha – yaloyokosa maisha! Lakini sasa najua kuna kizuri kimoja kimeletwa na hali hii, watu wamechoshwa, watu wameanza kusema, “Yesu hakuniokoa nikaye hapa nikauke, chini ya mchungaji ambaye anafanya kazi kama desturi tu ya kidini. Nipe Ukweli! Nipe Kristo!&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Nitawaeleza Sasa Kuhusa Yule Msalio – Mmoja Kati Ya Kumi Aliyegeuka Na Kumrudia Yesu!&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Ni kwanini kwamba katika kila uzazi kuna wale wanao mkimbilia Yesu kwa Shauku na Shukrani kuu? Kanini Mungu anakuwa kila mara na yule mmoja anayeacha yote na kurudi kumsifu na kumuabudu Kristo? – wengine asilimia 98 wakiendelea tu na desturi za kidini? Naamini Msamaria alimrudia Yesu kwa sababu hakuwa amefungwa na utamaduni wa wayahudi. Lakini Msamaria alipoona mikakati na desturi ya kidini alilia “La hapana! alishuhudia ufananisho feki uliokuwa na wale makuhani na waumini. Aliona wafarisayo wakiibia wajane na kuchukua nyumba zao. Aliona Makuhani wakipeana rushwna na kula rushwa. Aliona sinagogu lililojaa wafanyi biashara wakigeuza pesa, waliogeuza nyumba ya Mungu kuwa ukumbi wa wezi! Akaona waandishi wakitengeza sheria ya kufwatwa na watu wengine ingali wao hawakuinia hata kidole kimoja kizifuata! Aliona nyuso zilisopakwa “chokaa”, nyuso za uongo na zinazokosa usawa. Na akajiambia, “hapa naona vipofu wakiongoza vipofu – hapa hapanifai mimi, nataka ile Halisi!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Alipokuwa akielekea kule kijijini na wale tisa – kurudi kwa makuhani, kurudi kanisani, kwa jamii, heshima na maisha mazuri – alisimama na kufikiri: “ngoja kidogo” nakumbuka vile ilikuwa nilipokuwa na kila kitu – pesa, fahari, usalama. Jameni nilikuwa Mtule! Rafiki zangu wa dhati walinikana nilipowaeleza kwamba labda niko na Ukoma. Nilikuwa Upweke! – Mfungwa katika dhambi, aliyejaa chuki na uchungu moyoni, ilikuwa kama kuzimu! Kwanini nirudiye maisha hayo? Kisha kitu kilianza kumchoma moyoni: “hebu niangalie mimi – Nimekuwa msafi sasa, Yesu ameniponya! Kanisa litangoja kwanza – familia itangoja kwanza. Mimi naenda kwa Yesu! Nataka kumjua yule aliyeniponya! Aliafikia azimio ambalo Wasalia wengi hufikia: “hamna lolote kule nje ninalolitaka, yote ni bure! Mimi naenda kwa Yesu – Yeye ndiye atakuwa Ukweli wangu!”&lt;/p&gt;
&lt;div class=&quot;newsletter-highlight&quot;&gt;Usifikiri Kwa Dakika Moja Kwamba Mkoma Huyu Aliyetakaswa Alirudi Tu Kusema Asante – La, Alikuwa Amelemewa Na Tamaa Kuu Ya Kumuabudu Yesu&lt;/div&gt;
&lt;p&gt;Mkoma huyu Msalia hangeweza kukoma kulia, “Utukufu! Sifa zilibubujika kutoka ndani ya Nafsi yake. Ninaamini kuwa yeyete amuabuduye Kristo kama huyu mtu – akijilaza kufudifudi miguuni mwake, akilia bila kujizuia – huyo atakuwa ameamua kabisa kutomwacha Yesu tena! Moyoni mwake asema, “nitaenda kwa nani mwenigine? Yeye anayo maneno ya Uzima wa Milele! Tafakiri mtu huyu anapotokea kila mahali Yesu anapofunza, wakati Kristo akiwa kando ya mlima, ama kando ya bahari, hapo yupo yule Mkoma aliyetakaswa akiwika: “nakupenda Yesu! Utukufu kwa Mungu! Sifa Kwako!” Ninamuona mtu huyo Yesu alipokuwa akipaa Mbunguni akilia, “Yesu nichukue twende nawe!” Napenda kufikiri kuwa alikuwa katika chumba kile cha juu wakati wa Pentekosti akimsifu Mungu – akiwa amejazwa na Roho Mtakatifu!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Ukweli ni Kwamba, sisi tumepewa kitu ambacho huyu Mkoma mwenye shukurani hakuwa nacho. Uweza mkuu unao zidi nguvu zote zijulikanazo hapa ulimwenguni. Kila Januari, sisi Waamerika umtuza Rais kwa kiti kiitwacho, “Mamlaka yenye nguvu zaidi duniia nzima!” Sahihi yake ni sheria. Ana mamlaka juu ya Jeshi la nguvu zaidi duniani. Inambidi tu afinye tu kitufe kuleta maafa dunia nzima. Walakini, nguvu za Rais huyu, hazikaribiiani kamwe na Nguvu zile Yesu ametupatia mimi na wewe! Tazama tuko na fursa isiyo na kipimo kusongelea na kuja mbele za Muumba, Mungu Aliyehai – na pia Yeye kuja kwetu! &quot;Kwa hiyo, ndugu zangu, kwa kuwa tunao ujasiri wa kupaingia Patakatifu pa Patakatifu kwa damu ya Yesu, kwa njia mpya iliyo hai tuliyofunguliwa kwa ajili yetu kupitia kwenye lile pazia, yaani, mwili Wake, basi kwa kuwa tunaye kuhani mkuu juu ya nyumba ya Mungu, sisi na tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu kwa imani timilifu, mioyo yetu ikiwa imenyunyizwa damu ya Kisto na kuwa safi kutokana na dhamiri mbaya nayo miili yetu ikiwa imeoshwa kwa maji safi. &quot; (Waebrania 10:19-22).&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Huyu Mkoma hakuwa na Nguvu hizi zilizokuja pale pazia ya Hekalu ilipopasuliwa mara mbili. Mambo haya yalipotendeka, ilimaananisha kwamba binadam angeweza kuingia ndani na Mungu pia angeweza kutoka nje – kukutana nasi! Neno “Ujuba” hapa lina maanisha “Kuwa na Uwazi uliofichuliwa waziwazi”. Wapendwa, “Uwazi” huwo ni kwa sababu ya Shetani! Inamaana ya kwamba tunaweza kukemea mapepo yeyote kutoka kuzimu tukisema, “Nina Haki katika Damu ya Yesu kuingia katika Uwepo wa Mungu na kuongea Naye! – naye Mungu kuongea nami! Je unaamini kuwa uko na Haki hii? – kwamba Mungu yu tayari kutoka ili kukutana nawe? Basi tumsongelee Mungu na moyo uliojaa Imani! Hatuji kwa damu ya ndege, mbuzi au Ndume – lakini kwa Damu ya Bwana wetu Yesu! “Hakuingia kwa njia ya damu ya mbuzi na ya ndama, lakini aliingia Patakatifu pa Patakatifu mara moja tu kwa damu yake mwenyewe, akiisha kupata ukombozi wa milele. Damu ya mbuzi na ya mafahali na majivu ya mitamba vilivyonyunyiziwa wale waliokuwa najisi kwa taratibu za kiibada viliiwatakasa hata kuwaondolea uchafu wa nje. Basi si zaidi sana damu ya Kristo, ambaye kwa Roho wa milele alijitoa nafsi Yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na waa kutusafisha dhamiri zetu, kutokana na matendo yaletayo mauti, ili tupate kumtumikia Mungu aliye hai!” (Waebrania 9:12-14).&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Hakuna lile linalomfurahisha Mungu kama watoto wake wanao kuja kwake na Ujuba mkuu, bila uoga! Anataka tuje tukisema, “Nina Haki ya kuwa hapa! Na hata kama moyo wangu unanihukumu, Mungu ni Mkuu kuliko moyo wangu! (soma 1 Johana 3:20). Mkoma huyu alipomsongelea Yesu mara ya pili, Maandiko yanasema, Yesu “alimfanya Mkamilifu”. “Yesu akamwambia, “Inuka na uende zako, imani yako imekuponya.” Wakati huu Yesu alimbariki na jambo kuu kuliko tu Utakaso, alimbariki na Ukamilifu wa Akili, Mwili, Nafsi na Roho. Na hili ndilo Mungu anawapatia wote wamsongeleao siku ya Leo, Ukamilifu! Napenda kufikiri kwamba Mkoma huyu aliyefanywa kamili alirudi kijini na kuungana tena na wale wengine Tisa. Jameni ni mazungumzo ya ajabu kweli walikuwa nayo! Wale Tisa labda walianza kunena shida zile walizokumbana nazo waliporudi. Bibi zao walikuwa wamekwisha olewa na watu wengine, watoto waliwaepuka kwa aibu, marafiki wakitambo walijifanya wageni kwao, kujiendekeza kulikuwa na Uzito usiowezekana. Wakamgeukia yule Mkoma Msalia, “ilikuwa vipi upande wako?” unamkumbuka yule Mgalilea aliyetuponya? Je unajua habari zake? Na kwanini unakaa mwenye Furaha? Akatabasamu na kusema, “Nilikuwa naye haswa jana! Mimi namfuata yeye – nimekuwa mwanafunzi wake na yeye amekuwa Mwalimu wangu. Namuniamini, sijakuwa na shida ya kujiendekeza! Hainikeri moyo kwamba familia yangu ilinikana, au kwamba rafiki zangu walinikwepa, Yesu alinipokea! Ndugu zanguni hebu niwaambiye – mimi natembea na Mungu! Ananiongelesha na Ananifunza. Nimekuwa mtengeneza Hema sasa – lakini zawadi yangu kuu ni kumsifu Bwana wangu!&quot; labda aliwaalika wale Tisa wajiunge naye kwenda kwa Yesu. Lakini labda wangekataa hoja yake: “pole – tunasoma sheria mara tatu usiku kwa wiki. Tuko na hoja kali tunajadili sasa kuhusu lini Mwokozi wetu atakuja!” labda walifikiri wanamtafuta Mwokozi – lakini walikuwa washamkosa tayari! Basi huyu Mkoma Msalia alirudi kwa Yesu akiimba, “Kuna nyimbo moyoni mwangu hata Malaika hawawezi kuimba – Nimekombolewa, Nimekombolewa!” Anaishi kwa Ukombozi – amefanywa kamili – Huru kabisa!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Mpendwa mtakatifu, mimi na wewe tumebarkiwe na lile kuu kushinda lile alilokuwa nalo huyu Mkoma Msalia. Hatuna tu mlango wazi, lakini Baba mpendwa atuambiaye, “Njoo – Umetakaswa. Amini – Chukua azma kwa Imani. Njoo ukutane na Yesu!” Hallelujah!&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;---&lt;br /&gt;
(Maandiko yamenakiliwa kutoka kwa IBS-STL Global translation &lt;a href=&quot;http://www.ibs.org/bibles/swahili/index.php&quot;&gt;http://www.ibs.org/bibles/swahili/index.php&lt;/a&gt;)&lt;/p&gt;</description>
 <category domain="http://www.worldchallenge.org/sw/taxonomy/term/275">David Wilkerson</category>
 <pubDate>Fri, 02 May 2008 09:08:15 -0500</pubDate>
 <dc:creator>thomas_rewe</dc:creator>
 <guid isPermaLink="false">5777 at http://www.worldchallenge.org</guid>
</item>
</channel>
</rss>

