KISIOKUA KAWAIDA ‘KWA MAISHA YA KAWAIDA’
Wacha nikuambie jinsi Mungu huleta watu ndani ya nyumba yake, jinsi anaongea nao na jinsi anavyowaokoa. Bwana anajenga kanisa lake kupitia shuhuda za nuru inayoangaza kutoka kwa wale wampendao. Ana uwezo wa kufanya hivyo sio kwa sababu watumishi hawa hutumia njia sahihi lakini kwa sababu wanaishi maisha sahihi.